Serikali
 kupitia Mamlaka ya EPZ imetenga eneo lenye ukubwa wa Hekta 1,363 katika
 Mkoa wa Tanga kwa ajili ya ujenzi wa viwanda na uthamini wa eneo husika
 umekamilika.
Hayo
 yamesemwa Bungeni Jijini Dodoma wakati Waziri wa Uwekezaji, Mhe. 
Mary Nagu akijibu swali la Mhe. Omari Rashidi Nundu kwa niaba ya Waziri 
wa Viwanda na Biashara aliyetaka kujua ni matayarisho na utekelezaji upi
 unafanywa na Serikali  uweza kutekeleza azma hiyo katika kipindi cha 
mwaka 2010-2015 na ni nini hatma ya Viwanda vya zamani ambavyo kwa muda 
mrefu havifanyi kazi.
 Mhe.
 Nagu amesema kuwa mkakati wa kuufanya Mkoa wa Tanga kuwa jiji la 
viwanda upo katika hatua nzuri na kuongeza kuwa kwa hivi sasa viwanda 
vipya vilivyojengwa na vinavyojengwa ni pamoja na kiwanda cha NILCANT 
cha kutengeza chokaa, kiwanda cha Rhino Cement pamoja na kiwanda cha 
Sungura Cement ambacho kinatarajiwa kujengwa.
“Jiji
 la Tanga limeingia ubia na kampuni ya Korea (GoodPM) kwa ajili ya 
kutekeleza mradi mkubwa wa kujenga viwanda 15 katika eneo la ekari 73 
huko Pongwe unaotarajiwa kuanza mwezi Mei mwaka huu chini ya utaratibu 
wa Tanga Economic Corridor”. Alisema Waziri Nagu.
Akijibu
 swali la nyongeza toka kwa Mhe. Nundu lililotaka kujua kama Serikali 
iko tayari kufanya tathmini kufufua viwanda vya zamani, Waziri Nagu 
amesema kuwa Serikali inakubaliana na hilo na iko tayari kuhakikisha 
viwanda hivyo vinafufuliwa.
 Aidha
 Mhe. Nagu aliongeza kuwa Serikali ni moja hivyo itashirikiana na Wizara
 ya Viwanda kupitia Waziri wa Viwanda kuhakikisha kuwa viwanda vya 
zamani vinafufuliwa.
 
