Mkuu wa Mkoa wa Tanga Bibi Chiku Galawa akimkaribisha Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad katika Mkoa huo mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Tanga.
Makamu 
wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akisalimia na vikosi vya 
ulinzi na usalama pamoja na wananchi wa Mkoa wa Tanga, mara baada ya kuwasili 
katika uwanja wa ndege wa Tanga.
 Makamu 
wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akisalimia na wananchi 
mbali mbali waliojitokeza kumpokea wakati walipowasili katika uwanja wa ndege wa 
Tanga kwa ziara ya siku mbili. (Picha na Salmin Said, OMKR)
Makamu 
wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akisalimia na wananchi 
mbali mbali waliojitokeza kumpokea wakati walipowasili katika uwanja wa ndege wa 
Tanga kwa ziara ya siku mbili. (Picha na Salmin Said, OMKR)
Makamu 
wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad amesema wananchi 
wanahitaji kuelimishwa zaidi juu ya uhifadhi wa mazingira ili waweze kuyalinda 
na kuepuka kuyachafua.
Amesema 
uchafuzi wa mazingira mara nyingi umekuwa ukisababishwa na wananchi wenyewe, 
jambo ambalo linapaswa kupigwa vita kwa wananchi kupatiwa elimu ya mazingira ili 
kuepusha uharibifu huo.
Maalim 
Seif ameeleza hayo wakati akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Tanga bibi Chiku 
Galawa, mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Tanga kwa ziara ya siku 
mbili.
Amesema 
iwapo wananchi wataelimishwa ipasavyo wataweza kujiepusha na uharibifu wa 
mazingira, ikiwa ni pamoja na kukata miti kiholela bila ya kuzingatia athari za 
kimazingira.
Nae 
Mkuu wa Mkoa wa Tanga bibi Chiku Galawa amesema uharibifu wa mazingira ni moja 
kati ya changamoto kubwa zinazoukabili Mkoa huo, jambo ambalo linarejesha nyuma 
maendeleo ya kiuchumi katika Mkoa huo.
Amesema 
Serikali ya Mkoa huo inatafuta njia mbadala ya kutumia nishati nyengine ili 
kupunguza matumizi ya kuni ambayo yanachangia ukataji wa miti 
kiholela.
“Iwapo 
serikali itazuia matumizi ya makaa na kuni, serikali na wananchi watapata nafasi 
ya kufikiria nishati mbadala ya kutumia kwa ajili ya kupikia, lakini tukiendelea 
kutumia kuni mawazo yetu yatabakia hapo hapo tu na tutaendelea kutumia kuni kila 
siku”, alitanabahisha bibi Chiku.
Amesema 
ukataji wa miti kiholela katika Mkoa huo umekuwa ukichangia kuwepo kwa athari za 
mabadiliko ya tabianchi yanayopelekea kuweko kwa upungufu wa mvua pamoja na 
kuongezeka kwa hali ya joto.
Hata 
hivyo bibi Chiku amesema Mkoa huo umepiga hatua kimaendeleo, ikiwa ni pamoja na 
kuimarika kwa miundombinu ya barabara.
Akiwa 
Mkoani Tanga, Maalim Seif ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi CUF 
anatarajiwa kuhutubia mikutano mitatu ya hadhara katika viwanja vya Tangamano, 
Kwadiboma Sokoni na Handeni.
Hassan 
Hamad (OMKR)
 
