Hili ni darasa jipya lililojengwa sasa katika Shule ya Msingi Silabu iliyopo Wilaya ya Korogwe darasa hili linatumiwa na wanafunzi wa darasa la tatu
Mti huu kivuli chake ni ofisi ya walimu wa Shule ya Msingi Silabu iliyopo Wilaya ya Korogwe
Uchochoro huu ndio lililuwa darasa la tatu kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Silabu iliyopo Wilaya ya Korogwe
Na Mwandishi wa Thehabari.com Korogwe WALIMU wa Shule ya Msingi Silabu Wilayani Korogwe Mkoa wa Tanga bado wanatumia kivuli cha mti uliopo mbele ya shule hiyo kama ofisi ya walimu (staff room) kwa kukosa jengo la ofisi.
Hiki
 ni kipindi cha miezi sita imepita sasa tangu mtandao wa Thehabari.com uripoti habari
 hii mapema mwezi Agosti 2012.
Juzi mwandishi wa habari hizi alipita tena katika shule hiyo kuangalia 
juhudi za Serikali na wananchi kufanikisha ujenzi wa ofisi hiyo, lakini 
alishuhudia walimu wa shule hiyo wakiendelea kufanya shughuli zao chini 
ya mtimu. 
 “…Hii
 ndiyo ofisi yetu bado,jengo ambalo tutalitumia kama ofisi halijajegwa 
shuleni hapa, hivyo tunatumia kivuli cha mti huu kama ofisi na wakati 
mwingine jua likizidi huamia pembezoni mwa kingo za darasa lenye 
kivuli,” alisema mmoja wa walimu ambaye alikutwa amekaa chini ya mti 
huku akiendelea na kazi. 
Hata
 hivyo mwalimu huyo hakuwa tayari kutaja jina lake kwa madai si msemaji 
wa shule hiyo, juhudi za kumpata Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Silabu,
 Mizeki Charahani ziligonga ukuta baada ya kuambiwa alikuwa nje ya shule
 kikazi. 
Awali
 mwezi Agosti mwandishi wa habari hizi aliripoti wanafunzi wa darasa la 
tatu katika Shule hiyo kusomea kwenye uchochoro unaotenganisha kati ya 
darasa moja na lingine kutokana na uhaba wa vyumba vya madarasa.
Wanafunzi hao ambao darasa lao lilikuwa likihama kila muda kutengemea 
hali ya hewa (jua na mvua) kufuata kivuli walilazimika kusomea nje 
kwenye uchochoro ambao haujaezekwa kutokana na uhaba wa vyumba vya 
madarasa shuleni hapo. 
 Hata
 hivyo tayari limejengwa darasa moja ambalo kwa sasa linatumiwa na 
wanafunzi wa darasa la tatu, huku darasa la kwanza na la pili 
wakiendelea kusomea kwenye darasa moja kutokana na uhaba wa vyumba vya 
madarasa unaoikabili shule hiyo, yenye darasa la kwanza hadi la saba. 
*Imeandaliwa na www.thehabari.com 
 
 
No comments:
Post a Comment