WAKATI zimebakia saa 24 Tanzania kuungana na nchi nyingine 
duniani kuanza kurusha matangazo ya televisheni kwa mfumo wa Dijitali 
zikiachana na ule wa Analojia, imebainika kuwa mpango huo utaanzia Mkoa 
wa Dar es Salaam pekee.
Habari za ndani kutoka Mamlaka ya Mawasiliano 
Tanzania (TCRA), zilizolifikia Mwananchi Jumapili, zinaeleza kuwa Jiji 
la Dar es Salaam pekee, ndiyo litakuwa la kwanza kuingia kwenye mfumo 
huo kuanzia Januari mosi, 2013 na siyo mikoa mingine nchini.
TCRA, imeshatangaza kuwa itaufunga mfumo wa analojia ifikapo Desemba 31 mwaka huu yaani kesho.
TCRA, imeshatangaza kuwa itaufunga mfumo wa analojia ifikapo Desemba 31 mwaka huu yaani kesho.
Habari hizo zimeeleza kuwa mamlaka hiyo imeamua 
kuchukua hatua za tahadhari katika utekelezaji wa mpango huo muhimu, kwa
 kuanza na mji mmoja baada ya mwingine, ambapo  mwezi mmoja baada ya Dar
 es Salaam kuanza kutumia mfumo wa dijitali, utafuatia Mkoa wa Dodoma.
Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Profesa John Nkoma 
alipoulizwa aliliambia gazeti hili jana kwamba mamlaka yake itatoa 
ufafanuzi kuhusu suala hilo leo katika mkutano wake na waandishi wa 
habari.
“Hatuwezi kukurupuka katika suala hili, tuko 
makini, lakini kesho (leo), tutakuwa na mkutano wa wanahabari kwa ajili 
ya kueleza mikakati mbalimbali na jinsi tulivyojipanga katika jambo 
hili,” alisema Profesa Nkoma.
Tayari TCRA imetaja miji mingine mbali ya Dar es 
Salaam ambayo imeshaunganishwa katika mfumo wa dijitali kuwa ni pamoja 
na Arusha, Mwanza, Tanga, Mbeya, Moshi na kwa sasa mji wa Morogoro 
unajengewa miundombinu husika.
Habari zaidi zilieleza kuwa kwa utaratibu uliopo 
sasa itachukua miezi kadhaa kabla ya kuzimwa kwa mfumo wa analojia 
katika miji minane ya awali, ambapo pia itachukua muda mrefu zaidi 
kuzimwa mfumo huo nchi nzima.
Shirika la Kimataifa la Mawasiliano (ITU), 
limezitaka nchi zote duniani kuhamia kwenye mfumo huo wa kurusha 
matangazo ya televisheni wa dijitali kutoka mfumo wa analojia ifikapo 
Julai 2015.
Ikiwa nchi mwanachama wa Jumuiya ya Afrika ya 
Mashariki (EAC), Tanzania imeanza kutekeleza azimio la nchi hizo 
ilizozitaka kufanya hivyo mwaka huu wa 2012, badala ya kusubiri hadi 
tarehe ya mwisho iliyowekwa na ITU.  
Wakati Tanzania ikiwa mstari wa mbele kuhamia 
kwenye mfumo huo wa dijitali, ingawa kwa mtindo wa awamu, nchi nyingine 
wanachama wa EAC hasa Kenya na Uganda bado hazijaingia katika mfumo huo.
TCRA imezikabidhi kampuni tatu kufanya kazi ya 
usambazaji wa mfumo huo wa dijitali, ambazo ni Basic Transmissions  
inayoundwa na Kampuni za IPP Media na Sahara
Communications, Kampuni ya Ting ya Agape Associates na Star Media Tanzania Limited (Startimes) ambayo ina ubia na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) na Star Communications and Technology ya China.
Communications, Kampuni ya Ting ya Agape Associates na Star Media Tanzania Limited (Startimes) ambayo ina ubia na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) na Star Communications and Technology ya China.
TCRA imekuwa ikielezea kuwa Tanzania ipo tayari 
kujiunga na mfumo huo kwa kuwa asilimia kati ya 22 kati ya 24 ya nchi 
ambayo inatumia analojia, tayari imefikiwa na mtandao wa mfumo wa 
dijitali, ikijumuisha miji minane ambayo kwa kiasi kikubwa kampuni ya 
Startimes imeifikia.
Hata hivyo, utata bado unagubika urushaji huo wa chaneli za bure ambazo ni ITV, Star TV, TBC1, Channel Ten na Eat Africa TV ikielezwa kuwa wamiliki wa vituo hivyo hawataki zionyeshwe bure kwenye kila king’amuzi bali ving’amuzi vyao pekee.
Hata hivyo, utata bado unagubika urushaji huo wa chaneli za bure ambazo ni ITV, Star TV, TBC1, Channel Ten na Eat Africa TV ikielezwa kuwa wamiliki wa vituo hivyo hawataki zionyeshwe bure kwenye kila king’amuzi bali ving’amuzi vyao pekee.
 
 
No comments:
Post a Comment