Miss East Africa Jocelyne Maro 2012
Jocelyne
 Maro Miss East Africa Tanzania akipunga mkono kwa mashabiki wake mara 
baada ya kutangazwa mshindi katika shindano hilo lililofanyika usiku wa 
kuamkia leo kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam 
akiwashinda warembo wenzake kutoka mataifa mbalimbali ya Ukanda wa 
Afrika Mashariki na nchi Jirani na Ukanda huo.
Jocelyne
 Maro ni Mtanzania wa kwanza kushinda taji hilo tangu lililpoanzishwa,amejinyakulia zawadi zenye thamani ya dola za kimarekani 30,000 likiwemo
 Gari aina ya Toyota Verossa, mara baada ya majaji kumtangaza mrembo 
huyo ukumbi mzima ulilipuka kwa shangwe huku watu mbalimbali 
wakimpongeza kwa ushindi wake.
Miss East Africa Jocelyne Maro akipongezwa na wenzake mara baada ya kushinda katika shindano hilo.
Miss
 East Africa Jocelyne Maro akipiga picha ya pamoja na Miss Uganda Ayisha
 Nagudi mshindi wa pili katika shindano hilo kushoto na Miss Burundi 
Ariela Kwizera ambaye alipata nafasi ya tatu katika shindano hilo.
 
 
No comments:
Post a Comment