Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Kanisa Katoliki la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, akiendesha ibada takatifu ya kubariki mafuta ya Krisma na kurudiwa kwa kiapo cha mapadri, iliyofanyika katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Joseph, jana. Picha na Emmanuel Herman.
Kiongozi wa Kanisa  Katoliki nchini, Mwadhama Kardinali Polycarp
 Pengo, amewataka mapadri wa Kanisa hilo kuwa kioo kwa matendo mema kwa 
kila wanachokifanya kwa wengine.
Kardinali Pengo aliyasema hayo jana wakati wa misa
 ya sherehe ya Sakramenti ya Upadri na kubariki mafuta ya Pasaka katika 
Kanisa Kuu la Mtakatifu Joseph jijini humo.
Alisema ni lazima kuwa watimilifu wa kibinadamu 
kwa kupitia njia ya sadaka, mateso na kifo hivyo kuwataka kuwafundisha 
yaliyo mema na yenye kumpendeza Yesu Kristu.
“Ili kufikia ukamilifu hatuwezi kukwepa misalaba, 
waumini mnatakiwa kutuombea ili kuweza kumwakilisha Yesu Kristu kwa 
matendo yaliyo mema na ya kumpendeza,” alisema Kardinali Pengo. “Hivi 
sasa  shida na mahangaiko ya dunia ni mengi  lazima  kumwonyesha Yesu 
ili aweze kutusadia na kushinda.
“Tukianza kuangalia chanzo cha matatizo na 
mahangaiko yalivyo hivi sasa hatuwezi kufika na tutaangamia,” alisema 
Kardinali Pengo.
Alisema njia nyingine zozote ambazo zinashabikia 
kama anasa na ukatili haziwezi kufanikiwa, hivyo aliwataka Mapadri hao 
kuwahubiria amani waumini.
 
 
No comments:
Post a Comment