Prof Ninatubu Lema kutoka Chuo cha Uhandisi na Teknolojia (CoET), kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB)
WAZIRI wa Ujenzi, John Magufuli amemteua 
 Prof Ninatubu Lema kutoka Chuo cha Uhandisi na Teknolojia (CoET), kuwa 
Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB), uteuzi huo unaanzia 
Desemba 20 mwaka huu.
Kwa mujibu wa taarifa ya 
Magufuli iliyosambazwa kweye vyombo vya habari jijini Dar es Salaam 
jana, na kusainiwa na Kaimu Katibu Mkuu, Balozi Herbet Mrango, ilieleza 
kuwa uteuzi huo, utadumu kwa kipindi cha miaka mitatu hadi Desemba 20, 
2015.
Kwa mujibu wa sheria Na. 15 ya 
mwaka 1997 ya mabadiliko madogo ya sehemu ya 3(3) ya kifungu 1(1) (a), 
na 1(2), kama ilivyorekebishwa na Sheria Na. 24 ya mwaka 2007, ndiyo 
iliyomfanya Waziri afanye uteuzi wa wajumbe wa Bodi hiyo akiwemo 
mwenyekiti huyo.
Katika uteuzi huo, Magufuli pia 
aliwataja wajumbe wanane wa bodi hiyo ya ERB, kuwa ni pamoja na Fintan 
Kilowoko kutoka wizara hiyo, ambapo kwa sasa ni mkurugenzi wa Barabara 
za Mikoa, Joseph Malongo, ambaye kwa sasa ni Msajili Msaidizi Huduma za 
Usajili na Gemma Modu kutoka Baraza la taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE),
 Nuberis Nyange kutoka Chama cha Wahandisi Washauri nchini (ACET).
Wengine ni Sarah Barahamoka, 
kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Edwin Ngonyani kutoka 
Wizara ya Nishati na Madini, Prof Bakari Mwinyiwiwa; Mhandisi 
Mwandamizi, Chuo cha Uhandisi na Teknolojia (CoET), kutoka Chuo Kikuu 
cha Dar es salaam na Prof. John Kandoro; Mkuu wa Taasisi ya Teknolojia 
Dar es Salaam (DIT).
Waziri alisema kuwa jukumu la 
msingi la Bodi hiyo ya Usajili wa Wahandisi ni kusajili wahandisi pamoja
 na Kampuni zinazotoa ushauri wa kihandisi, kuendeleza wahandisi 
kitaaluma, kuwajengea uwezo wa Wahandisi wa kitanzania.
 
 
No comments:
Post a Comment