MUUNGANO wa Makanisa nchini 
unatarajia kufanya Mkesha wa kuliombea Taifa ili amani na utulivu uliopo
 uweze kudumu, ambao unatarajiwa kufanyika Desemba 31 mwaka huu kwenye 
viwanja vya Taifa jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na wandishi wa habari 
jijini Dar es Salaam leo, Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi, Godfrey 
Malassy , alisema mkesha huo umekuwa ukifanyika kila Desemba 31 ya kila 
mwaka, kuukaribisha mwaka mpya.
Alisema lengo la mkesha huo ni 
kuliombea Taifa hilo mungu, ili aweze kuliponya na kulinusuru na majanga
 mbalimbali, na kudumisha amani miongoni mwa jamii yote nchini.
Malassy aliongeza kuwa Taifa kwa
 sasa linapita katika kipindi kigumu hususani kuanzia uelewa, uchumi, na
 katika masuala ya usalama wa raia wa ndani na nje ya nchi ambapo kuna 
baadhi ya watu wameanza kuichezea amani kwa kusababisha vurugu kwa 
kvisingizio vya dini.
Pia alisema kuwa Watanzania 
wanapaswa kudumisha amani na utulivu kwani hiyo ni tunu ambaayo 
wamepatiwa na mungu hivyo haipaswi kuchezewa na watu wachache wasio na 
nia njema.
“Mkesha wa dua hilo, utafanyika 
Desemba 31 mwaka huu kuanzia saa 2:00 usiku hadi asubuhi katika viwanja 
vya Taifa Dar es Salaam, na tunatarajia Rais Jakaya Kikwete atakuwa 
mmoja wa wageni wetu waalikwa” alisema Malassy.
Malassy alibainisha kuwa mkesha 
huo wa maombezi utashirikisha mikoa zaidi ya 16 ya Tanzania Bra na 
Visiwani, ambapo utakuwa na lengo la kuwaleta Watanzania kuliombea Taifa
 kwa ajili ya kudumisha amani, umoja na mshikamano visitetereke.
 
 
No comments:
Post a Comment