JUMUIYA ya wanataaluma wa Kiislamu nchini (Tampro), imesema kwa kushirikiana na taasisi nyingine, inaandaa mpango mkakati wa kuhakikisha inawasaidia vijana wanaosoma katika shule za sekondari za Kata ili waweze kufanya vizuri katika mitihani yao ya mwisho kama sehemu ya jitihada zao kwa jamii ya Watanzania.
Akizungumza kuhusu  maazimio ya 
mkutano mkuu wa jumuiya hiyo uliomalizika juzi katika hotel ya Lamada 
jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji Jumuiya hiyo Sadiki Gogo, 
alisema wamefikia uamuzi huo baada ya kuridhika na utafiti ilioufanya na
 kubaini kuna haja ya wao kama wanataaluma kutafuta njia ya kuwasaidia 
vijana hao kimasomo.
”Tampro kupitia kliniki 
yake ya Elimu, iliomba na kupata kibali Wizarani cha kufanya utafiti 
katika shule kadhaa za sekondari za kata hapa nchini na kugundua kuwa 
zina uwezo wa kufanya vizuri iwapo zitasaidiwa katika baadhi ya nyanja” alisema Gogo
Akifafanua baadhi ya nyanja 
hizo, Mkurugenzi  huyo, alisema  pamoja na kuwapa mafunzo maalum walimu 
wa shule hizo na baadae kupeleka walimu wa kujitolea katika baadhi ya 
shule zitakazoonekana zina upungufu mkubwa.
Sambamba na mkakati huo ambao 
amedai unalenga kuisaidia serikali, Gogo alisema Tampro kupitia mkutano 
huo imeazimia kuanzisha vituo vya Elimu maalum pamoja na huduma 
nyinginezo kwa watu wenye mahitaji maalum kama vile ya ulemavu.
Aidha Mkutano mkuu huo umeazimia
 kushirikiana na wadau wengine nchini kuwekeza katika sekta ya Afya kwa 
madai kuwa bila ya kuwa na watu wenye afya zilizoimarika ,ni ngumu Taifa
 kufikia maendeleo ya kisiasa na kiuchumi.
 
 
No comments:
Post a Comment