Tuesday, January 29, 2013

MUHIMU:::TUSIBEZE TAHADHARI YA MVUA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgh4CL4lD5LoA2aIBpKspBS9GJp_9MBRehN-elzmcwc8e1_Fx8SB2bWInUJ9sOG6Nc-KaKeRetmprw-Elc_SN9d1AzN1Ntn1gE6dQN3WcKpeT6D8EZx2N7PhgxZNU0hAQkKYkoVkQ-BBFE/s1600/FELLENG.jpg

Taarifa kuhusu uwezekano wa matukio ya Mvua kubwa (zaidi ya milimita 50 katika kipindi cha saa 24 kila siku) katika baadhi ya maeneo ya mikoa  ya Rukwa, Iringa, Mbeya, Njombe, Ruvuma, Morogoro, Pwani, Lindi, Mtwara  na maeneo jirani ya mikoa hiyo kati ya tarehe 30 Januari, 2013 hadi 01 Februari, 2013.
Hali hii inatokana na kuwepo kwa kimbunga “FELLENG” kaskazini-mashariki mwa Madagascar ambacho kinavuta upepo wenye unyevunyevu kutoka Congo kupitia maeneo tajwa.