Saturday, December 22, 2012

TAIFA STARS YAWAKANDAMIZA MABINGWA WA AFRIKA 'CHIPOLOPOLO' 1-0 UWANJA WA TAIFA DAR ES SALAAM

MATOKEO YA MPIRA WA MIGUU KATI YA TAIFA STARS NA CHIPOLOPOLO LEO MARA BAADA YA DAKIKA TISINI


   
Hivi ndivyo Usomekavyo Ubao wa Matokeo katika Uwanja huu wa Taifa jijini Dar es Salaam kwa kipindi cha kwanza cha mchezo katika ta Taifa Stars na Mabingwa wa Afrika,Zambia wana Chipolopolo.kipindi cha kwanza kimemalizika sasa huku Taifa Stars ikiongoza kwa bao moja lililotiwa kimiani na Mrisho Ngassa mnamo dakika 45 ya mchezo kipindi cha kwanza.


 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgpZ6aUbT4o04TBSs8BpqWjqGMhQCpTSz1x7ZeXUzPV_HwxwkjbjxEyC0waFEVvrXEf2HgOL0c7EbMkINTjMh_VaB2CDG3LB0SFmizfX-eY6TB5ybCgRS6lki74BFJa_mhnAWlGZjOG8VYt/s1600/IMG_3775.jpg


Mrisho Ngassa mnamo dakika 45 ya mchezo kipindi cha kwanza akiachia shuti kali lililoizawadia Tanzania ushindi.


 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgjghy00fU-50cuFCXJ5etDzrCGJDv0U-SXwSgw3AKw7gMNcBQ7MLAK8GiNtehla9ZQX24nfalhbLC7YUZ6gPkg2SB_xoHn6vON7ZIT0TLB2XBP6znZPnlJj-_OAYAPo1Wdj87hH4UiPlds/s1600/8.jpg


Mashabiki wa Timu ya Taifa ya Tanzania wakishangilia Ushindi wa timu yao.


 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEipI1-MKzm8KDKukaKRh_FXRCfxvnukvPw1giDzy9_MrxkG0Ly6KlHsBacm-pP4nKhaivTM9PJfmaaMFOuyFVWNhKWyH9TQvAs1K2IgUiONoWx92YZNyfmtHeF7s2wD1StFAdcd7OjFscWf/s1600/IMG_3791.jpg

kocha wa Taifa Stars Kim  Poulsen akipeana mkono na kocha wa Chipolopolo ambaye alionekana kutofurahishwa na matokeo ya mchezo.

Jocelyne Maro Mtanzania wa kwanza kushinda Miss East Africa 2012 katika shindano hilo lililofanyika usiku wa kuamkia leo kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam

Miss East Africa Jocelyne Maro 2012

  
Jocelyne Maro Miss East Africa Tanzania akipunga mkono kwa mashabiki wake mara baada ya kutangazwa mshindi katika shindano hilo lililofanyika usiku wa kuamkia leo kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam akiwashinda warembo wenzake kutoka mataifa mbalimbali ya Ukanda wa Afrika Mashariki na nchi Jirani na Ukanda huo.
Jocelyne Maro ni Mtanzania wa kwanza kushinda taji hilo tangu lililpoanzishwa,amejinyakulia zawadi zenye thamani ya dola za kimarekani 30,000 likiwemo Gari aina ya Toyota Verossa, mara baada ya majaji kumtangaza mrembo huyo ukumbi mzima ulilipuka kwa shangwe huku watu mbalimbali wakimpongeza kwa ushindi wake.


 m
  
Miss East Africa Jocelyne Maro akipongezwa na wenzake mara baada ya kushinda katika shindano hilo.


 o

  
Miss East Africa Jocelyne Maro akipiga picha ya pamoja na Miss Uganda Ayisha Nagudi mshindi wa pili katika shindano hilo kushoto na Miss Burundi Ariela Kwizera ambaye alipata nafasi ya tatu katika shindano hilo.