Sunday, October 28, 2012

Chuo cha kiislam cha Zahrau cha jijini Tanga, kipo eneo la madina

l
Chuo cha kiislam cha Zahrau cha jijini Tanga

Eckernforde Tanga University(ETU)

  • Street: Tanga
  • Country: Tanzania
  • Region: Tanga 
  • ADDRESS: P.O.Box 5032 PHONE NUMBER(S): +255 27 2646144  www.eckernfordtangauniversity.ac.tz

Friday, October 26, 2012

TANZANIA: Sanaa Iletayo Uzima

 https://encrypted-tbn3.gstatic.com/images?q=tbn:ANd9GcQ2Ibzgz90pRYwR3q-wR5pu4pDKQXpJa7-YsR5soXg7-zn8G3ft
mabasi mapya kabisa ambayo yanafanya safari zake Dar na Pangani

Marko Gideon

PANGANI, TANGA, Julai 15, 2011  (IPS) - Pangani siyo wilaya mpya
 nchini Tanzania. Wengi wanatambua wilaya ya Pangani kuwa moja ya
wilaya zilizoanzishwa miaka mingi na moja ya vitovu vya ukoloni
na biashara nchini Tanzania. Mji wa Pangani uliopo katika eneo
Mto Pangani unapomwaga maji yake katika Bahari ya Hindi, upo
umbali wa takribani Kilomita 42 kutoka Tanga mjini.

Unapoingia katika mji wa Pangani unapokelewa na vitu vingi
 ambavyo kama ni mgeni lazima utashangaa. Miongoni mwa vitu hivyo
ni majengo ya zamani ambayo yana historia ya ukoloni. Moja ya
majengo hayo ni lile linalotumika kama ofisi ya Mkuu wa Wilaya
hiyo. Umbali wa takribani mita mia mbili kutoka ofisi ya Mkuu wa Wilaya katika
mji huu mdogo unaokadiriwa kuwa na wakazi elfu hamsini, unakutana
na mandhari nzuri ya Mto Pangani unavyomwaga maji yake katika
Bahari ya Hindi. Kandokando mwa mto huo mkubwa kuna barabara
ambayo imepangiliwa vizuri pamoja na kwamba imejaa mashimo ambayo
yanaashiria lami iliyotengenezwa wakati wa zama za mkoloni. Pia kuna majengo na bustani ambapo vyote hivyo vimepangiliwa vizuri na kuleta mandhari ya kupendeza ya mji huo mkongwe nchini.

 Mbali na Mto Pangani na kuona majengo ya zamani, mgeni pia
ataona mabango yamebandikwa katika maeneo mbalimbali ya mji huo
yakiwa na nembo ya UZIKWASA. Neno hili linasimama badala ya
shirika lisilokuwa la kiserikali katika wilaya hiyo lijulikanalo
kama Uzima kwa Sanaa.
 
TCMP ni shirika linalofanya kazi kwa kushirikiana na Kituo cha
 Rasilimali za Pwani na Bahari (Coastal Resource Centre) chini ya
Chuo Kikuu cha Rhode Island nchini Marekani, serikali ya Tanzania
chini ya Shirika la Usimamizi wa Mazingira Tanzania (NEMC) na
kufadhiliwa kwa kiasi kikubwa na Shirika la Misaada ya Maendeleo
ya Kimataifa la Marekani (USAID).

 Pengine siyo jambo la kushangaza kuona kuwa wengi nchini
 Tanzania wanahusisha suala zima la sanaa na uchezaji ngoma na
pengine michezo ya kuigiza au uchoraji. Lakini UZIKWASA
inatafsiri tofauti ya dhana hiyo ya sanaa.

 Ndani ya moja ya ofisi zake tatu zilizopo kandokando mwa Mto
 Pangani, shirika hilo limetandaza machapisho mbalimbali kuhusu
VVU na UKIMWI, elimu ya uzazi na kujamiiana kwa vijana, matumizi
ya kondomu, elimu ya malaria kwa watoto na wajawazito, magonjwa
ya ngono na ushauri nasaha na kupima VVU – yote haya yakifanya
kazi ya kuonyesha jinsi gani sanaa inaweza kuleta uzima.

 Kwa mfano, unaweza kushuhudia machapisho yenye vichwa vya
 habari kama vile "Maswali waliyouliza vijana kuhusu UKIMWI na
kizazi kipya", "Maswali waliyouliza vijana kuhusu mimba",
Mahusiano kati ya mwanaume na mwanamke", "Maswali waliyouliza
vijana kuhusu mahusiano ya kimwili", Maswali waliyouliza vijana
kuhusu matumizi ya kondomu", Walinde watoto na wajawazito dhidi
ya malaria", "Yafahamu magonjwa ya ngono na athari zake", "Mbinu
maalum za kumpa kijana kupambana na maisha", "Kuzuia maambukizo
ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto", "Fahamu ushauri nasaha
na kuchunguzwa maambukizo ya VVU na chapisho juu ya elimu ya
"Kuingia utu uzima".

 Haya yote yanatoa picha kuwa UZIKWASA siyo shirika la
 kufundisha uchezaji wa ngoma, bali linatumia aina zote za sanaa
ili kulinda maisha ya mwanadamu hasa vijana wa kike na wa kiume.

 Moja ya shughuli za UZIKWASA ni kukabiliana na maambukizo ya
 VVU/UKIMWI katika vijiji vya wilaya ya Pangani. Kazi hii
hufanywa kwa kushirikiana kwa karibu na wananchi wa vijiji chini
ya Kamati za UKIMWI za Vijiji (Village Multi-sectoral AIDS
Committees-VMAC). Na moja ya shughuli za shirika hapa ni kutoa
elimu ya jinsi ya kukabiliana na VVU/UKIMWI na pia kusambaza
kondomu kwa walengwa ambao miongoni mwao ni pamoja na kundi la
wavuvi ambalo linaonekana kuwa katika hatari ya kuambukizwa
VVU/UKIMWI kutokana na asili ya kazi zao.

 Kazi zao zinawafanya kuwa mbali na nyumbani kwa muda mrefu
 ambapo huishi kwenye makambi. Wavuvi wa kiume na kike wanapokuwa
makambini wanaweza kuanzisha tabia hatarishi,Tabia hatarishi pia zinaweza
kujitokeza wakati wavuvi wa kiume wanapokutana na wanawake na mabinti wanaokwenda kununua samaki kwa ajili ya uchuuzi."


 Utafiti wa kubainisha maeneo yanayosambaza kondomu ulioendeshwa
 na UZIKWASA uliweza kujua nani wanauza kondomu, idadi ya kondomu
zinazouzwa kwa siku, kwa nini wengine hawauzi kondomu na kama
wanapenda kuuza siku zijazo.

 UZIKWASA imepata mafanikio katika eneo hili. Kulingana na
 maofisa wake viongozi wa kidini wanaonekana kukubali kuwa
VVU/UKIMWI haina dini. Hii imewafanya wasiendelee kuhubiri tena
dhidi ya kondomu wala kutetea matumizi yake.

 "Wameendelea kuhubiri maadili mema kama njia nyingine ya
 kujikinga na VVU/UKIMWI bila kugusia masuala ya matumizi ya
kondomu," anasema Urassa. Pia usiri uliogubika suala zima la
kuongelea kondomu mbele ya umma umeanza kuondoka. Kwa kiasi sasa
watu wanaweza kusimama mbele ya umati na kuendelea kuchangia
katika mjadala unaohusu matumizi ya kondomu.

 Sanaa inayoleta uhai haishii kwenye kupambana na magonjwa
 pekee, lakini pia kwenye kusaidia shughuli za kuongeza kipato
ili wananchi waweze kuendesha maisha yao bila shida. Hapa
unakutana na mradi wa Vikundi vya Kuweka na Kukopa (SACCOs). Kwa
sasa UZIKWASA inalenga katika kuhakikisha kuwa makundi yenye
matatizo zaidi katika jamii kama vile walemavu, yatima, wajane na
watu wanaoishi na virusi vya UKIMWI yanajengewa uwezo wa
kuanzisha SACCOs zao au kujiunga na SACCOs zilizopo.

KUMBUKUMBU YA MAREHEMU GORDON

KUMBUKUMBU
YA
MAREHEMU GORDON KALLISTO HAULE

 

Tarehe 27/10/2012 umetimiza miaka minne(4) tangu roho yako ilipotengana na mwili wako,ndugu zako mama yetu mpendwa Annuciata Mwingira Haule,Deogratias,Deograsia,Godwin,Killian,Annamaria,Agness,Kallistus pamoja na jamaa na rafiki zako tunakukumbuka kwa sala na ibada.Tunamuomba MUNGU akurehemu na akujalie raha na nuru ya milele pamoja na watakatifu wake,amina!.


Thursday, October 25, 2012

Bidhaa mbovu za mamilioni zimeteketezwa Tanga

 https://encrypted-tbn1.gstatic.com/images?q=tbn:ANd9GcSpn9qRNrd-Bi6ms828JKLA-I-rYsm4-JbEDmYFuCtSA6g2nNee
Raisa Said,Tanga.
HALMASHAURI ya  Jiji la   Tanga,  imeziteketeza  dawa, vipodozi  na bidhaa za vyakula ambavyo muda wa kutumiwa kwake, umekwisha.Kwa pamoja, bidhaa hizo zina thamani ya  Sh. 13.908,730.

 Akizungumza  na waandishi  wa habari mara  baada  ya  tukio hilo,  Kaimu  Mfamasia  wa Jiji  la  Tangam Abdillah Mnenge,  alisema dawa hizo zilikamatwa kutoka kwa wafanyabiashara mbalimbali wa jijini hapa .

Mnenge alisema  uteketezaji wa dawa hizo, ulifanyika juzi katika dampo kubwa lililoko Duga Maforoni na kwamba ulisimamiwa na wataalamu kutoka katika halmashauri ya Jiji na askari polisi.
Aliiomba Serikali kupitia Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) kuimarisha mipaka na ukaguzi ili kudhibiti uingizwaji wa vipodozi haramu hapa nchini.

Pia aliviomba vyombo vya habari hapa nchini, kutoa elimu juu ya madhara ya utumiaji wa bidhaa ambazo si rafiki wa binadamu na zilivyokwisha muda wake.

Kaimu Mfamasia huyo alisema wataendelea kuimarisha i ukaguzi kila baada ya miezi mitatu katika maeneo yote ya Halmashauri ya Jiji la Tanga, ili kudhibiti uingizwaji wa bidhaa zilizokwisha muda wake.

Agricultural Research Institute (ARI) Mlingano

Historical background
ARI – Mlingano was established in 1934 with the objective to conduct research for improvement of sisal yield. Since then Mlingano has remained a household name for sisal growers. Nearly all sisal varieties grown in the country were developed at Mlingano. At present Mlingano has a collection of over 120 varieties of sisal (the largest collection in the world)
For users of soil information ARI – Mlingano is always the first place to consult in matters related to natural resource management, soil and land resources and fertilizer use technology. Nearly all activities in the country related to land evaluation and land use planning, fertilizer recommendations, agro ecological zones and soil analysis have had a connection with ARI – Mlingano.
Location
ARI- Mlingano is located 15 km from Muheza town on the highway to Tanga. Mlingano is a humid place with a bimodal type of rainfall (1150mm per annum).
Staff Strength
ARI- Mlingano has a strong team of 24 agricultural research scientists (7 PhDs, 7 MSc and 8 BSc). Our scientists have frequently been involved in collaborative research and consultancies requested by assorted National, Regional and International institutions such as SUA, NEMC, TANRIC (DSM). ASARECA, SADDC, FAO, UNDP, UNIDO, AGRIS. (KIT- The Netherlands ).
RESEARCH ACTIVITIES
Sisal Research Read notes on Tanzania agro ecological zones in Pdf and in Word
Main activities covered under sisal research are variety evaluation, agronomy, and plant protection. Lack of good quality planting materials for the growing sisal industry led to establishment of the meristematic tissue culture (MTC) laboratory at ARI-Mlingano in 2000. Establishment of the tissue culture laboratory was financed by Common Funds for Commodities (CFC) and United Nations Industrial and Development Organization (UNIDO). The laboratory is aimed at multiplying good sisal plants which are high yielding and uniform materials. The sisal materials multiplied by tissue culture will be established in estate nurseries which will serve as multiplication centers for planting materials. Read notes on rainfed agriculture crop suitability for Tanzania

https://encrypted-tbn1.gstatic.com/images?q=tbn:ANd9GcR-cD4pQRl-dG9D10t7LdvGsI_qtDfEaBIXnmmUkbWHEhL6JkmAfQ
 Dr.Adolf Nyaki(right) & Dr.Jeremias Mowo(left)

Soil Research
During the early days of the institute soil research covered mainly analytical services and development of fertilizer packages for the sisal industry which was then supported by the Tanzania Sisal Growers Association (TSGA).
Soil and Land Resource Surveys
In the early 1970s soil research was expanded to address a Nationwide project called National Soil Service (NSS) which was supported by UNDP and executed by FAO from 1974 – 1984. During this period several districts were surveyed including Sengerema, Geita and Dodoma at scale that ranged between 1:125,000 and 1:250,000. The present country soil and Physiography and Agroecological zones maps were produced during that period. During the period 1984 and 1994 the famous soils program refered to as “NSS” was supported by the Dutch Government. During this time several other districts were surveyed and most of the detailed soil appraisals were carried out including most of sisal estates. Other activities completed during the project period were surveying of Mbulu, Morogoro Rural, Biharamulo, Kahama and Maswa districts.
The purpose of soil and land resources suitability assessment are diverse depending on the request put forward but in general it involves identification of biophysical and social-economic constrains that causes low productivity and therefore recommend interventions that enable sustainable land use planning for increased productivity.
Click here to see soils and physiography Map or Click here to see Agro-ecological zone Map
Approaches
There has been an evolution of techniques used in Land Resources Surveys as technologies in science change world-wide. Recently for example there are applications of Geographical information Systems (GIS) and Remote Sensing (RS). The use covers land degradation assessment, land resource inventories, agro- ecological zonations, land suitability assessment and farming systems zonation.
The farming systems zonation has recently been realized as an important undertaking at all levels for planning, targeting and delivery of agricultural services and new technologies that aim at reducing poverty and improving crops and livestock production in order to improve people's livelihood. The farming system zonation involves identification and taking into consideration all the physical characteristics and the social-economic attributes of the region under consideration. The farming systems approach (FSA) enables an integrated approach in agricultural development and hence efficient use of scarce resources and effective delivery of services to various stakeholders and minimizes duplications of efforts. Although, the country wide coverage has been accomplished the eastern zone is more comprehensive while updating is planned for the remaining zones.
Soil Fertility and Conservation research
Soil fertility constraints and development of soil fertilizer use technology are among research activities carried out at national level. In 1983 a country wide fertilizer recommendation guide based on broad Agroecological zones and on district by district basis was compiled. The guide indicates fertilizers requirement per crop, per type of soil in every part of the country.
Research activities going on currently include use of leguminous cover crops ( Canvalia spp, Dolicos lablab and Mucuna spp ) to improve soil productivity. Several agroforestry trees including Greillea, Gliricidia, Jacarana, Senna spp, Moringa, Acacia etc. These are being evaluated for soil fertility improvement and supply of fuel wood as well as other uses which are increasingly becoming a problem in highly populated areas.
The institute is also doing research to recommended soil conservation techniques. Recent studies carried out in Lushoto indicated that water erosion removes up to 100 tones of soil per hectare per year, which can be considered as very high losses. This amount could be reduced to less than 1 ton per hectare if conservation measures such as fanya juu, bench terraces are adopted.
Soil and Plant Analytical Laboratory
The soils laboratory at ARI Mlingano has a national mandate, with a capacity of analysing over 5000 soil and plant samples annually. Soil samples are analysed for the purpose of characterization, classification and land evaluation for the purpose of mapping, soil fertility appraisal, monitoring and provision of advisory services. It is a member of LABEX, an international quality control organization for agricultural laboratories. The soil testing and GIS Laboratories have just been rehabilitated through PADEP under the support of the Word Bank.
Capacity Building Activities
ARI- Mlingano conducts tailor – made training programs to a wide range of clients in agriculture related enterprises. Some of the tailor- made training programmes fall in the following fields:
    • Soil and plant analysis and management of agricultural laboratories
    • Soil survey and soil mapping
    • Land evaluation
    • GIS applications in natural resources management
    • Fertilizer application
    • Sisal cultivation
    • Soil and water conservation
    • Remote sensing and aerial photo interpretation.
Scientists seeking to improve their skills in these and related fields are always welcome.
Contracts and consultancy assignments
Mlingano has been active in contract or demand driven assignments. These covered a wide range including soil surveys and land evaluation for multiple uses, farming systems, impact assessments and contract research with district councils meant to solving low productivity problems. Examples of these types of assignments include
•  Development of refinement of fertilizers recommendations for maize and rice in Kilombero district, and Kagera transboundary agro-ecosystems management project for FAO - Tanzania
Click here to see Mombo Irrigation Scheme
Click here to see Kagera agro-ecosystems map in Kagera River Basin
Contacts
ARI MLINGANO, P.O.Box 5088 , TANGA Tel: +255-27-2647647 Fax: +255-27-2642577

Watumishi 15 Kilindi wapata msukosuku wa ubadhirifu

 https://encrypted-tbn0.gstatic.com/images?q=tbn:ANd9GcSbG9_EpcP0JDXBHXeQHky95ZATx8UL95Acdh_StyPdX1s2weMT
Hussein Semdoe, Kilindi
BARAZA la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi ,mkoani Tanga, limewafuta kazi watumishi wawili  kati ya 15 wa halmashauri hiyo waliokuwa wakikambiliwa na utata wa ubadhirifu.

Watumishi wengine watatu kati ya hao wamevuliwa madaraka yao kwa madai ya kutiwa hatiani kwa makosa mbalimbali yaliyoisababishia hasara Serikali.
Watumishi hao waliochukuliwa hatua hizo ni miongoni mwa wafanyakazi 15, wa halmashauri hiyo, waliokuwa wakihusishwa na tuhuma za ubadhirifu wa fedha za umma.
Madiwani hao walifikia uamuzi huo mwishoni mwa wiki katika kikao cha halmashauri hiyo maarufu kwa jina la ‘Waseuta Nougone’, kilichofanyika chini ya Mwenyekiti wake Mussa Semdoe na Mkurugenzi Mtendaji Daudi Mayeji.

Awali, katika mkutano huo, Ofisa Utumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi, Pascal Lefi, aliwasilisha taarifa ya kamati ya uchunguzi wa watumishi waliokuwa na tuhuma mbalimbali kwa niaba ya Mkurugenzi, na kutaja majina ya watumishi 10 waliokuwa wamefunguliwa mashtaka ya nidhamu.
“Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi ilikumbwa na tuhuma za ubadhilifu wa fedha za umma, hali iliyofanya uongozi  kuomba kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali kuja kufanya ukaguzi maalumu, kwa hesabu za mwaka 2008, 2009 na 2010. Baada ya kukamilika ukaguzi huo jumla ya watumishi 15 walihusishwa na tuhuma hizo,” ilieleza sehemu ya taarifa hiyo na kuongeza.
“Matokeo ya ukaguzi huo yamefanya watumishi watano wasimamishwe kazi na kupelekwa katika vyombo vya dola ama sheria, wengine wanne walisimamishwa kazi kupisha uchunguzi na watumishi wengine sita waliendelea na kazi huku tuhuma zikiendelea,” alisema Mkurugenzi huyo.
Mayeji aliwataja watumishi waliofutwa kazi kuwa ni Robert Kwayi, aliyekuwa ni mhasibu, ambaye ametiwa hatiani na kamati hiyo, kutokana na uzembe uliosababisha halmashauri hiyo kupata hasara ya Sh 80 milioni, na Edward Kapwapwa, ambaye ni Afisa Kilimo Msaidizi, aliyetimuliwa kazi kutokana na utoro kazini.
Aliwataja maofisa waliovuliwa madaraka, kuwa ni pamoja na, Fredrick Kiango, aliyekuwa Afisa Kilimo na mifugo wa Wilaya ya Kilindi, ambaye amekutwa na hatia ya Uzembe uliosababisha wilaya hiyo kupata hasara ya Sh 80 milioni, kwa kushindwa kushauri vizuri katika ununuzi wa Power Tiller zilizokuwa na upungufu.

Eid al-Adha in 2012 is on Friday, the 26th of October.

 
Millions of pilgrims head to Mina as hajj 2012 officially kicks off


Note that in the Muslim calander, a holiday begins on the sunset of the previous day, so observing Muslims will celebrate Eid al-Adha on the sunset of Thursday, the 25th of October.
Although Eid al-Adha is always on the same day of the Islamic calendar, the date on the Gregorian calendar varies from year to year, since the Gregorian calendar is a solar calendar and the Islamic calendar is a lunar calendar. This difference means Eid al-Adha moves in the Gregorian calendar approximately 11 days every year. The date of Eid al-Adha may also vary from country to country depending on whether the moon has been sighted or not.
The dates provided here are based on the dates adopted by the Fiqh Council of North America for the celebration of Eid al-Adha. Note that these dates are based on astronomical calculations to affirm each date, and not on the actual sighting of the moon with the naked eyes. This approach is accepted by many, but is still being hotly debated.

mashindano mpira wa Kikapu ya kombe la Taifa, yanatarajiwa kufanyika mjini Tanga kuanzia Oktoba 29 hadi Novemba 4, mwaka huu 2012.

 https://encrypted-tbn3.gstatic.com/images?q=tbn:ANd9GcSVjte3yBXT5vuQKPnbJTy2VylkaaMX2t3R5BalXkgq5NrWI9ukjw
mashindano haya ya Kombe la Taifa kwa kawaida ndio hutumika kuchagua timu zetu za Taifa, hvyo ni muhimu kwa mikoa yote kushiriki ili kuwapa nafasi wanamichezo kutoka mikoa yao kuonekana katika ngazi ya Taifa.mikoa iliyothibitisha hadi sasa ni Iringa, Mbeya, Arusha, Kilimanjaro, Shinyanga, Singida, Mara, Dodoma, Pemba, Unguja, Tanga, Mtwara, Lindi na Dar Es Salaam.

Tuesday, October 23, 2012

In 1988; Soni Seminary of CATHOLIC DIOCESE OF TANGA took the first position National wise in Form IV National Exam Results.


SOME COOL BEHIND THE SCENE,THE BEST TANGA RECORD


http://www.dioceseoftanga.org/pages_inswahili/offices/education/soniseminary/soniseminary2.jpg


 http://www.dioceseoftanga.org/pages_inswahili/offices/education/soniseminary/soniseminary3.jpg

 http://www.dioceseoftanga.org/pages_inswahili/offices/education/soniseminary/soniseminary1.jpg

 http://www.dioceseoftanga.org/pages_inswahili/offices/education/soniseminary/soniseminary5.jpg

 http://www.dioceseoftanga.org/pages_inswahili/offices/education/soniseminary/soniseminary4.jpg

 http://www.dioceseoftanga.org/pages_inswahili/offices/education/soniseminary/soniseminary6.jpg

In 1978 Fr. Ndunguru was sent to Dar es Salam University for further studies in teaching. Fr. Maganga took the leadership of Soni Seminary as Rector. After finishing his studies Fr. Ndunguru came back to Soni Seminary as Rector and Teacher up to 1988 when Fr. George Mhuza took his position as Teacher and Rector. Fr. George was coming from Dar es Salam University where he hired his degree in education. He became Rector for 10 years. In 1998 his position was taken by Fr. Fraternus Mbuya. Since 1998 up to 2005 Soni had different leaders who served for a very short time. These are, Fr. Fraternus Mbuya, Gerald Kabarega, Severine Msemwa, Benedict Shemfumbwa and Fr. Thomas Kiangio who started his career since 2005.
The Patron Saint was changed in the year 1979 from Saint Michael to Saint Joseph the Husband of Mary. St. Joseph was prefered due to his role in taking care of the child Jesus so as to take the same role of caring of the young Seminarians in their eary stage of formation. It was also in the same year the first form four did National Exams and came out with good results, which proved that the staff was doing a good job. Since 1979 form four result has been giving hope to the Bishop as well as the faithful of Tanga Diocese. In 1988; Soni Seminary took the first positin National wise in Form IV National Exam Results. More than that, there has been also a lot of development in buildings and in 1996 Soni had students who did form VI exams. These A-level classes were stopped in the year 1998. Now effort is made to bring back A-level classes.

Benki ya NMB Lushoto.

https://encrypted-tbn3.gstatic.com/images?q=tbn:ANd9GcS8cgF8E-Tpkj6TjBelFhHrdSHo2bcWM9LjWfIKs-J5qiGWnlvQ

TBL Yadhamiria Kujenga Visima Handeni

Mkurugenzi wa Uhusiano na Sheria wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Steve Kilindo amemkabidhi Diwani wa Kata ya Kwamgwe, wilayani Handeni, Tanga, Shariffa Abebe mfano wa hundi yenye thamani ya sh. mil. 40.5 kwa ajili ya ujenzi wa visima.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjh5KCbqkB1juk7a79uBcBadC3Zi8g8D2DP_mPRnj1JLDfJu32J1mA4-cAFxeV2SY2a_v2dif92e7YLjguhddO0S_cJgHFXR_Fcftg3Jmx8zYmo3azZtdu7qTV2rAfGYoWSOMLONCeGum5_/s400/safirri6.jpg

Maktaba iliyopo kijiji cha Lushongo wilaya ya Pangani

Mohammed Dar Muasisi wa jina la Tanzania aliyesahaulika

Saumu Mwalimu
UNAPOTAJA historia ya nchi Tanzania, ni dhahiri kwamba hutaacha kutaja majina ya wapigania uhuru na viongozi mbalimbali walioiongoza tangu enzi za ukoloni, hadi kupata uhuru.
Hata hivyo, katika kila historia ya taifa lolote iliyojengwa, kuna watu waliofanikisha historia hiyo, lakini kwa sababu moja au nyingine, michango ya baadhi yao imesahaulika na pengine kutotajwa kabisa kwenye historia hizo.
Wengi wa Watanzania tunafahamu kuwa jina la nchi yetu Tanzania, limetokana na majina ya nchi mbili zilizoungana na kuwa moja ambazo ni Tanganyika na Zanzibar. Hivi ndivyo tulivyofundishwa shuleni.
Wengine wanaamini kuwa Rais wa kwanza na muasisi wa taifa hili, Hayati Mwalimu Julius Nyerere ndiye aliyebuni jina la Tanzania.
Lakini ukweli ni kwamba, jina la Tanzania lilibuniwa na mmoja wa wananchi walioshiriki mchakato wa kutafuta jina la nchi hii, baadaya muungano wa Tanganyika na Zanzibar mwaka 1964.
Mohammed Iqbal Dar ndiye aliyebuni jina la Tanzania, wakati huo akiwa na umri wa miaka 18 akiwa mwanafunzi wa Shule ya Sekondari  Mzumbe.
Ilikuwaje?
 “Nilikuwa maktaba najisomea, nilishika gazeti la Daily News, wakati huo likiitwa The Standard, ndipo nikaona tangazo hilo,” anaeleza Dar alivyopata hamasa na kuongeza:
“Siku hiyo hiyo, nikafanya majaribio ya kutafuta jina bila hata ya kuishirikisha familia yangu. Nilichuka karatasi na kalamu, lakini kabla sijaanza kufanya chochote, nilimwomba Mungu aniwezeshe kwa maana naamini Mungu, ndiye kila kitu wakati wa kufanya jambo lolote.”
“Kwa hiyo kwenye ile karatasi nikaandika Tanganyika na Zanzibar kisha, nikaandika majina yangu mawili;  Iqbal na Ahmadiya,” anasema Dar na kufafanua kuwa Iqbal ni jina lake na jina la ubini na  Ahmadiyya ndiyo dhehebu lake.
Kupata jina Tanzania
Akisimulia alivyopata jina Tanzania, anasema kuwa ilimchukua dakika tano tu kufikiria na kulipata jina hilo.
“Nilichukua Tan kutoka kwenye Tanganyika na kuongeza Zan kutoka kwenye Zanzibar na kupata Tanzan, niliona halitimii vizuri,”anasimulia Dar.
Anabainisha kuwa baadaye alifikiria na kugundua kuwa majina mengi ya nchi za Afrika yanaishia na IA mfano akitoa mfano wa Ethiopia, Gambia, Tunisia, Nigeria, Algeria, Somalia, Zambia, Namibia na kwamba baada ya kubaini hilo aliamua kuongezea herufi hizo mbili na kupata jina Tanzania.
“NIlituma maombi yangu katika shindano hilo, bila kumwambia mtu yeyote nyumbani,” anasema Dar.
Baada ya muda mfupi baba yake, mzee Tufail Ahmad Dar, alipokea barua kutoka Wizara ya Habari na Utalii (wakati huo), ambapo ndani yake kulikuwa na ujumbe wa pongezi ya kwamba kijana wake ameshinda katika shindano hilo.
“Wakati naandika, sikuwa na matumaini kama nitashinda kwa kuwa shindano hilo lilikua wazi kwa watu mbalimbali, hivyo sikuwa na tarajio lolote kama ningeshinda,
“Jioni wakati narudi nyumbani, baba mzazi alinifungulia mlango wakati si kawaida yake kwani mama ndiye alikuwa akinifungulia siku zote, hapo nikajua kuna kitu hakipo sawa. Lakini, nilikaribishwa na tabasamu la baba, pamoja na pongezi nyingi, nilifurahi sana,” anaeleza.
Tuzo
Dar anasema kuwa kwa ushindi huo, alitunukiwa ngao pamoja na fedha taslimu Sh200 kama zawadi ya ubunifu wake.
Pamoja na kuibuka mshindi wa ubunifu huo na hadi leo jina la Tanzania alilolibuni yeye linaendelea kutumika, lakini Dar anadai kuwa mchango wake huo kwa taifa ni kama hautambuliwi na Serikali imemsahau katika kuandika historia ya taifa la Tanzania.
“Sijui kwa nini sitambuliwi tangu wakati huo? Hakuna chochote kinachoelezea uhusika wangu katika kupata jina la Tanzania na ukiwauliza watu, wengi watakwambia ilikuwa ni Nyerere aliyeleta jina Tanzania, hii inaumiza,” anasema akilalamika.
Tanzania ya sasa
Baada ya miaka 13 tangu kufariki kwa Nyerere,  Dar anasema kuwa Tanzania haimtendei haki mwasisi huyo wa Taifa, ambalo ni kisiwa cha amani.
“Ni kama imepita miaka mingi sana tangu kifo chake. Watanzania wamesahau kila kitu alichokiota Mwalimu Nyerere. Nakumbuka moja ya vita kubwa aliyopigana ni dhidi ya rushwa, yeye aliichuki rushwa lakini kwa sasa, rushwa imekua kama ndiyo tafsiri ya maisha ya Tanzania. Hakuna kitu kinachoweza kufanyika kwa urahisi hata kama ni haki ya mtu, bila kutoa rushwa,” anasema.
Anaongeza kuwa: “Mwalimu Nyerere alikua ni rafiki ya baba yangu na walikua wakionana na kuongea, nakumbuka siku moja kulikuwa na sherehe nyumbani na kwa kuwa tulikuwa watoto, nilimhudumia chai Mwalimu.
“Nakumbuka Mwalimu aliwahi kumuuliza baba yangu; Lini Malaria itaisha nchini hii? Baba alimjibu kuwa, kamwe malaria haitaisha ikiwa hakutakuwa na kujitolea kwa kila mmoja wetu, bila kumtegea mwengine,” anasema.
Katika kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, Dar anaishauri Tanzania iendeleze misingi ya maisha ambayo Hayati Mwalimu Nyerere aliisimmamia, ikiwamo umoja na mashikamano, ili kuondoa tofauti kubwa kati ya maskini na matajiri.
“Tunaona namna ambavyo matajiri wanendelea kuwa tajiri zaidi, wakati maskini wanazidi kudidimia. Kama kungekuwa na ushirikiano kati ya watu hawa wawili, tofauti kati yao ingekuwa ndogo au isingekuepo kabisa,” anaeleza.
Anashauri pia kuwepo na sanamu za utambulisho ya Baba wa Taifa kila mahali, ili kulienzi jina lake liishi milele. “Kwa ninavyomjua Mwalimu natamani jina lake liishi milele na litangazwe lijulikane dunia nzima,”anasema.
Mohammed Iqbal Dar aliazaliwa mwaka 1944 jijini Tanga, ni mtoto wa tatu kati ya watoto saba wa Tufail Ahmad Dar.
Dar ni baba wa mtoto mmoja, ambapo kwa zaidi ya miaka 40 sasa amekuwa akiishi nchini Uingereza alikoenda kwa ajili ya kusoma kabla ya kuwa raia wa nchi hiyo.
Mbunifu huyo wa jina la Tanzania ni Mhandisi wa Masuala ya Redio, kazi anayoifanya nchini Uingereza, akieleza kuwa katika kuienzi nchi yake, nyumba yake iliyopo mjini Birmingham, ameipa jina la Dar es Salaam, ikiwakilisha ubini wake, pamoja na Jiji la Dar es Salaam.

Monday, October 8, 2012

mabadiliko ya Tabia nchi

 http://www.mwananchi.co.tz/images/stories/00000000000000000000pangani.jpg
 ATHARI za mabadiliko ya Tabia nchi zinaendelea kujidhihirisha katika maeneo mbalimbali hapa nchini ukiwemo mji wa Pangani. Mji wa Pangani upo katika mwinuko wa mita 0 hadi  100 kutoka usawa wa bahari. Ni moja kati ya miji inayoathirika  na mabadiliko ya Tabia nchi ambapo mbali na kuongezeka kwa joto, ongezeko la kina cha maji limekuwa ni tishio kubwa kwa wakazi wa mji wa Pangani na mali zao.

Saturday, October 6, 2012

ASKOFU NA KADINALI WA KWANZA KATIKA BARA LA AFRIKA AMEZIKWA TENA LEO KATIKA KANISA KUU LA MJINI BUKOBA


 
MAREHEMU LAUREAN RUGAMBWA



http://www.mwananchi.co.tz/images/stories/0000000000000001aazikwa.jpg

Mwili wa marehemu Rugambwa ambaye alikuwa Askofu na Kardinali wa kwanza Mwafrika alifariki dunia Desemba 8, 1997 na mwili wake kuhifadhiwa katika Kanisa la kwanza la Katoliki mkoani Kagera, Kashozi, hapa ukipelekwa kuzikwa rasmi katika Kanisa Kuu la Bukoba alilochagua yeye.


 KANISA ALILOZIKWA TENA ASKOFU

UHABA WA MAJI BADO NI TATIZO SANA WILAYA YA HANDENI HASA ENEO LA NJIA PANDA MKATA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjexXt9Kwo_z634r5DoSB5fNeX4wv21YMBti2-_eCrTRZD9YgxXVJaxJz7TaxNyKF14LZVwgTqh5zyBDJmjInyTeafVNAJzaZYHKAXJX0ByRWWZx_OUwrsNzvJ8lPyGhZyrvletrLAYki4/s1600/IMG_8404.jpghttps://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiq2mvhTysPtSmuJ1WP00D1AgC3T0tFSW_wuB9PxnfEz6eG9ng4BAgeVOMjr5FrVnTY7-oPBvPH5IO6g6Ij86MKaOQjMrjpBmB8RdEfICfzwJoBWRiGpaupmXRqpFzyJ38wsQ1bhHJ3S_Y/s1600/IMG_8338.jpghttps://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiXL-9vHxa0__Tw4vyvkMvshG-rgKHJCndHGKMI3hvFoBbiRkbT_k1f2z2mKMMIam9yicYWSFtEBTb9fnr3FNpGDQjp3TB0i_tRGhcnnxJuiQrZqB4wBQsPktotx5GVmE6F4zeJx5LzZkU/s1600/IMG_8336.jpghttps://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhe5AmxMIFY7uGV3Ak-6DwFzMCn_8k5DQGQxFpEjzGda7uYHOZrnbvurJO3DYQmVbJHDIvnrGSbXqFVr1sIB43awN1uQMzzcUAhBIs41FRKsIBTqHfYQZG1vy1NXoY1EsRpCRnnMdY7kg0/s1600/IMG_8331.jpg

Thursday, October 4, 2012

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MTIHANI WA KIDATO CHA NNE NA MTIHANI WA MAARIFA OKTOBA, 2012

Ndugu Wananchi,
Mtihani wa Kidato cha Nne mwaka 2012 utafanyika nchini kote kuanzia tarehe 08, hadi tarehe 25 Oktoba, 2012. Jumla ya watahiniwa walioandikishwa kufanya mtihani ni 481,414 wakiwemo wavulana 263,202 sawa na asilimia 54.67 na wasichana 218,212 sawa na asilimia 45.33. Idadi hiyo ya watahiniwa wote walioandikishwa mwaka 2012 ni ongezeko la watahiniwa 31,090 sawa na asilimia 6.90 ikilinganishwa na watahiniwa 450,324 walioandikishwa kufanya mtihani huo mwaka 2011.  Watahiniwa wote walioandikishwa kufanya mtihani mwaka 2012 wamegawanyika katika makundi matatu kama ifuatavyo:-
·         Watahiniwa wa shule (School Candidates) ni 412,594 wakiwemo wavulana 228,991 sawa na asilimia 55.50 na wasichana 183,603 sawa na asilimia 44.50.  Watahiniwa hao wa shule wa mwaka 2012 ni ongezeko la watahiniwa 63,204 sawa na asilimia 18.09 ikilinganishwa na watahiniwa wa shule  349,390 wa mwaka 2011.
·         Watahiniwa wa Kujitegemea (Private Candidates) ni 68,820 wakiwemo wanaume 34,211 sawa na asilimia 49.71 na wanawake 34,609 sawa na asilimia 50.29. Watahiniwa wa Kujitegenea walioandikishwa mwaka 2012 ni pungufu ya Watahiniwa 32,114 sawa na upungufu wa asilimia 31.82 ikilinganishwa na watahiniwa 100,934 walioondikishwa mwaka 2011.
·         Mtihani wa Maarifa (Qualifying Test) utafanyika tarehe 16 Oktoba, 2012. Jumla ya watahiniwa wa Mtihani wa Maarifa walioandikishwa ni 21,314 wakiwemo wanaume 8,174 sawa na asilimia 38.35  na wanawake 13,140 sawa na asilimia 61.65. Watahiniwa wa Maarifa walioandikishwa mwaka 2012 ni pungufu ya watahiniwa 8,133 sawa na upungufu wa asilimia 27.62 ikilinganishwa na watahiniwa 29,447 walioandikishwa mwaka 2011. 
Watahiniwa wote wameandikishwa katika shule/vituo vilivyotawanyika katika Mikoa mbalimbali nchini kama ifuatavyo:-  Jumla ya shule 4,155 zina Watahiniwa wa Shule (School Candidates).   Watahiniwa wa Kujitegemea (Private candidates) wameandikishwa katika vituo 902; na Watahiniwa wa Maarifa (Qualifying Test) wameandikishwa katika vituo 616.
Ndugu wananchi,
Hadi sasa maandalizi na usafirishaji wa mitihani hiyo hadi ngazi ya mikoa yamekamilika. Aidha, mikoa inaendelea na taratibu za kuhakikisha kuwa kila kituo kinapata mitihani yake kwa muda uliopangwa kwa kuzingatia taratibu na maelekezo ya Baraza la Mitihani la Tanzania.
Ndugu Wananchi,
Kuhusu usalama wa mitihani, hadi sasa mitihani yote ipo salama, na hakuna mtihani uliyovuja katika ngazi yoyote kuanzia Baraza la Mitihani, Mikoa na Halmashauri. Ninatoa pongezi kwa Baraza la Mitihani kwa kuandaa mitihani hiyo na kuisafirisha kwa usalama hadi ngazi ya mkoa. 
Ninatoa wito kwa Kamati za Mitihani za mikoa yote kuhakikisha kuwa taratibu zote za utunzaji, uhifadhi na usafirishaji wa mitihani hiyo zinazingatiwa. Ni matumaini yangu kuwa ufuatiliaji na ukaguzi wa usalama wa kila kituo umefanyika na hatua za kurekebisha mapungufu kama yapo zimefanyika.
Ndugu Wananchi, 
Mtihani wa Kidato cha Nne ni muhimu sana kwa wanafunzi na jamii kwa ujumla, kwani hutumika katika uchaguzi wa watahiniwa wanajiounga na masomo ya Kidato cha Tano na Vyuo mbalimbali.  Aidha, ili kuweza kujiunga na soko la ajira katika taasisi za umma au sekta binafsi ni lazima mhusika awe na cheti cha Kidato cha Nne.  Hivyo mtihani wa Kidato cha Nne ni muhimu sana kwa maisha ya watahiniwa na wananchi kwa ujumla.
Ndugu wananchi
Ufanisi wa zoezi muhimu kama la mitihani unahitaji ushirikiano wa wadau wote. Ninatoa wito kwa wananchi wote, wakiwemo Viongozi, walimu, Wazazi, Jamii na  Wasimamizi wa mitihani kutoa ushirikiano wa kutosha na kuhakikisha kuwa mazingira yanakuwa ya amani na utulivu kipindi chote cha mitihani. Wakuu wote wa vituo vya mitihani hakikisheni kuwa mahitaji yote ya msingi kuhusu mitihani yanapatikana. 
Ndugu Wananchi,
Kutokana na muhimu wa mtihani wa Kidato cha Nne katika  kutoa mwelekeo wa  maisha ya watahiniwa kama ilivyofafanuliwa hapo juu, wapo baadhi ya watahiniwa na wasimamizi wasio waaminifu ambao wamekuwa wakijihusisha na vitendo vya udanganyifu katika mitihani.  Watahiniwa wanaobainika kufanya udanganyifu katika mitihani wamekuwa wakifutiwa matokeo yao yote ya mitihani kwa mujibu wa Kanuni za Uendeshaji wa Mitihani ya Taifa. 
Ninachukua fursa hii kuwakumbusha watahiniwa kuwa, kila mtahiniwa afanye mitihani yake kwa kujitegemea bila udanganyifu. Wale wote watakaobainika kushiriki katika udanganyifu watachukuliwa hatua za kinidhamu. Nikirejea mtihani wa mwaka 2011, jumla ya watahiniwa wa Kidato cha Nne 3,303 walifutiwa matokeo yao kwa sababu ya kufanya udanganyifu. Aidha, walimu waliohusika walipewa adhabu mbalimbali ikiwemo onyo, karipio kali, kuvuliwa madaraka wakuu wa shule na wengine kushitakiwa TSD. Aidha, wenye shule waliothibitika kusababisha udanganyifu wameandikiwa barua ya kusudio la kuzuia kudahili wanafunzi wa Kidato cha Kwanza kwa muda wa mwaka mmoja. 
Kuhusu watahiniwa waliofutiwa matokeo, baada ya kuomba msamaha wamepunguziwa adhabu, na wataruhusiwa kufanya mtihani mwaka 2013 kama watahiniwa wa kujitegemea baada ya kutumikia adhabu kwa muda wa miaka miwili. Ninatoa wito kwa walimu, viongozi na wazazi kuwaasa watahiniwa kuhusu swala la udanganyifu, kwani kwa mwaka huu adhabu haitapunguzwa. Ni matumaini yangu kuwa watahiniwa wote watazingatia taratibu zote za mitihani bila kujiingiza katika udanganyifu. Serikali haitasita kuchukua hatua kama ilivyokuwa mwaka 2012.
Ndugu Wananchi,
Ninarudia kutoa wito kuwa walimu, wasimamizi wa mtihani, Wakuu wa Shule, viongozi wote, na jamii kutoa ushirikiano na kuhakikisha kuwa mitihani inafanyika katika mazingira yenye usalama na amani.  Ninaomba wote tuungane kuwaombea Watahiniwa wetu Baraka za Mwenyezi Mungu na mafanikio katika mitihani yao.
Ndugu Wananchi,
Katika kuhitimisha taarifa yangu ninapenda pia kutoa ufafanuzi kuhusu Mtihani wa Taifa wa Kidato cha sita kwa wanafunzi walioko kidato hicho mwaka 2012/2013. Wanafunzi hao watafanya Mtihani wa Taifa mwezi Machi, 2013. Aidha, wanafunzi waliopo kidato cha 3 mwaka huu watafanya Mtihani wa Taifa wa kidato cha 4 mwezi Novemba 2013 kama ilivyoelekezwa na Kamishna wa Elimu kwenye Waraka wa Elimu Na. 5 wa Mwaka 2012 kuhusu Marekebisho ya Mihula ya Shule za Sekondari na Vyuo vya Ualimu.
  
PHILIPO A. MULUGO (Mb.)
NAIBU  WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI