Tuesday, February 5, 2013

elimu yetu inavyojenga matabaka katika jamii.


 wanafunzi wa shule ya msingi wakiwa darasani,hii ndio tofauti kubwa kati ya shule yenye kutoa maarifa na ujuzi na shule yenye kutoa vyeti na sifa za kumuwezesha mtu kupata kazi.


MATOKEO mazuri au mabaya  ya elimu kwa mtu,  huonekana katika namna anavyotenda mambo na dhamira yake ya kutenda,  na wala hayatokani na alichojifunza, namna alivojifunza na sababu ya kujifunza.
Hiyo ndio tofauti kubwa kati ya shule yenye kutoa maarifa na ujuzi na shule yenye kutoa vyeti na sifa za kumuwezesha mtu kupata kazi.
Watu wengine wanapozungumzia elimu wanafikiri kuhusu utaratibu mzima wa kujifunza wenye lengo la kumpatia mtu ujuzi na maarifa na kumudu vyema kile alichojifunza.
Ujuzi na maaarifa ndio hasa lengo na upatikanaji wake  unaotarajiwa utumike katika kupambana na changamoto na hata kuibua na kuleta maarifa mengine zaidi.
Kuna watu wengine wanapozungumzia elimu,  wanafikiria umiliki wa cheti kinachoonyesha una ujuzi fulani.
Elimu ya aina hii sio kwa ajili ya kutumika katika maisha wala kutafuta maarifa mengine,  bali ni kwa ajili ya mtu kukariri anachojifunza na  kuyatoa yale maarifa yaliyokaririwa katika mitihani ili apate cheti kizuri kitakachowezesha kupata kazi yenye kipato kizuri.
Kimsingi,  cheti kazi yake ni kumpatia mtu kazi. Cheti ndio ‘pasipoti’ ya kwenda katika nchi ya kipato.
Watanzania wengi kama sio wote,  tumeangukia katika kundi hili. Wengi wetu tunataka pasipoti ya kwenda katika ‘nchi’ ya kipato cha kuajiriwa, tunataka vyeti!
Katika mfumo wetu wa elimu mpaka sasa ufaulu wa mtihani ndio unaosema fulani apangiwe shule gani, apangiwe kozi gani  chuoni, apate kiasi gani kwenye mikopo ya elimu ya juu na apangiwe kazi gani na alipwe kiasi gani.
Sasa kuna vita kati yetu, kila mmoja anataka mwanawe, yeye mwenyewe au ndugu yake  afaulu ili afike katika nchi ya ahadi.
Mbinu mbalimbali zinatumika  kufanikisha lengo hili, vita haina macho! Mbinu kuu ikiwa matumizi ya pesa. Kusoma shule nzuri na ghali, kulipia twisheni, walimu bora, kununua vitabu na mwishowe hata kununua mitihani.
Mchakamchaka  huu wa kutaka kufaulu kisha kupata vyeti,  unawaacha nyuma watu wa kipato cha chini kwani hawawezi kumudu kununua mitihani, au kusoma twisheni  za gharama.
Wenye nacho wananeemeka na mtindo huu. Mwelekeo unaonyesha masikini  wataachwa kwa kiasi kikubwa na wenye uwezo.
Mwanzo wa kujenga matabaka mawili kupitia elimu bila kificho  unaonekana.

Alhamisi hii feb 7,2013 kwenye AMPLIFAYA Clouds Fm.

Alhamisi hii feb7 2013 kuanzia saa moja usiku kwenye AMPLIFAYA ya CLOUDS FM dakika 120 zitatumika kuirusha Exclusive interview ya BABU WA LOLIONDO, ni safari iliyochukua dakika 570 kutoka Arusha mjini, ni zaidi ya saa masaa tisa(9).
Safari ya kwenda kwa Babu wa Loliondo Samunge ilianza kwenye defender ya polisi kwa sababu magari ya watu binafsi yalikua yanagoma kwenda kutokana na vita kali ya Wasonjo na Wamasai, hivyo njia pekee ya kufika kwa Babu ni kusindikizwa na Polisi, stori kamili ni Alhamisi hii feb 7 2013 kwenye AMPLIFAYA Clouds Fm.
Kwenye interview ya zaidi ya dakika 60 na Babu wa Loliondo Ambilikile, picha na stori nyingine zitapatikana kwenye millardayo.com kuanzia jumatano usiku na alhamisi.

kikao kazi cha maafisa habari wa serikali Dodoma

Picha na 1 f90c5Waziri wa Habari, Vijana ,Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara akifungua mkutano wa maafisa Habari, Elimu na Mawasiliano wa serikali mjini Dodoma. Pamoja na mambo mengine amewataka kufanya kazi  kwa kuzingatia weledi na kutoa taarifa sahihi kwa umma mara kwa mara kuhusu shughuli mbalimbali zinazofanywa na serikali.


Picha no 8 03ec7
 Mmiliki na muendeshaji wa mtandao wahabari na matukio wa Mjengwa Blog kutoka Iringa Bw. Maggid Mjengwa akitoa mada kwa maafisa Habari, Elimu na Mawasiliano wa serikali kuhusu Faida na Changamoto za matumizi ya mitandao ya kijamii kwa Mawasiliano Serikalini mjini Dodoma.


Picha na 7 f660a
Maafisa Mawasiliano wa Serikali wakiendelea na kikao kazi chao kujadili masuala mbalimbali ya utendaji kazi Mjini Dodoma.


Picha na 2 5c000
Maafisa Habari, Elimu na Mawasiliano wa Serikali wakiwa katika picha ya pamoja naWaziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo mara baada ya ufunguzi wa kikao kazi hicho  mjini Dodoma.


Picha na 3 958db
Afisa Habari wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi wa Hesabuza Serikali  Sarah Reuben akichangia moja ya mada katika kikao kazi cha Maafisa Habari, Elimu na Mawasiliano wa Serikali mjini Dodoma.


hab1 55f16
Baadhi ya maafisa habari wa serikali wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiAwasilishwa katika mkutano huo. Kutoka kulia ni Bw. Peter Millanzi mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Bw. Midradji Maez, Mkuu wa kitengo cha mawasiliano Shirika la Reli Tanzania (TRL) na Bw. Abel Ngapemba, Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano Shiririka la Maendeleo la Taifa NDC


hab2 6bb7f
. Maafisa Habari kutoka wilaya na Mikoa mbalimbali waliohudhuria kikao kazi cha maafisa habari mjini Dodoma wakiwa katika majadiliano ya pamoja kuhusu mafanikio na changamoto zinzoyakabili maeneo yao ya kazi.


hab3 bf999
Maafisa Habari kutoka wizara mbalimbali waliohudhuria kikao kazi cha maafisa habari mjini Dodoma wakiwa katika majadiliano ya vikundi kuhusu mafanikio na changamoto zinazoyakabili maeneo yao ya kazi wakiongozwa na mwenyekiti wa kikundi hicho Luteni Kanali Juma Sipe, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano.


hab 50c83
Meneja Mawasiliano wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Bw. Innocent Mungy akiwasilisha mada kuhusu mkakati wa Mawasiliano wakati wa Kikao kazi cha maafisa habari wa serikali kinachoendelea mjini Dodoma.

5/2/2013, Dodoma
Kikao kazi cha Maafisa habari wa Serikali kutoka Wizara, taasisi, wakala wa serikali, mashirika ya umma, mikoa na wilaya mbalimbali nchini leo kimeingia siku ya pili mjini Dodoma kwa  maafisa hao kupata fursa ya kujadili changamoto zinazokabili vitengo vya  habari na mawasiliano serikalini na namna ya kuzitatua.
Katika kikao hicho mada mbalimbali zimewasilishwa ikiwemo ile ya Mwongozo wa Ofisi za Mawasiliano serikalini iliyowasilishwa na Mkurugenzi wa Msaidizi kutoka Idara ya Habari (MAELEZO) anayeshughulikia uratibu wa vitengo vya mawasiliano serikalini akitoa msisitizo mkubwa  kwa maafisa habari kuyafahamu vizuri majukumu yao ya kazi kwa mujibu wa taratibu za utumishi wa umma ili kuboresha utendaji wa kazi.
 Pia maafisa hao wamepata fursa ya kujifunza namna ya kuboresha  mawasiliano serikalini kupitia mada ya mkakati wa mawasiliano (Communication Strategy) wa kuiwezesha jamii kupata taarifa sahihi kwa muda muafaka ,mada iliyowasilishwa na Meneja mawasiliano kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Bw. Innocent Mungy.
Katika mada hiyo Bw. Mungy ametoa wito kwa maafisa hao kuzitumia nafasi zao kutoa taarifa kwa umma mara kwa mara ili kuwapa fursa wananchi kufahamu yale yanayofanywa na serikali.
Ametoa wito maafisa hao kushirikiana na vyombo mbalimbali vya habari katika kutekeleza mkakati huo kwa kuhakikisha kuwa wanatoa habari kwa umma kupitia radio, magazeti, televisheni na mitandao ya kijamii ili kuepusha madhara yanayoweza ku.sababishwa na jamii kukosa taarifa sahihi za serikali za utekelezaji wa mipango mbalimbali ya maendeleo