Sunday, December 23, 2012

JIWE WALILOLIKATAA WAASHI LIMEKUWA JIWE KUU LA PEMBENI

 Lema anatisha sana Arusha

http://www.mwananchi.co.tz/image/view/-/1650374/medRes/440620/-/maxh/240/maxw/460/-/515gk2/-/lema.jpg

HABARI LEO


MTANZANIA
 

TANZANIA DAIMA
 

NIPASHE
 

MWANANCHI
 

MAJIRA
 

Kontena la kondom mbovu lakamatwa

zimebainika kwamba zipo madukani
KONTENA lililosheheni kondomu za kiume kutoka nchini India imekamatwa na kuzuiliwa katika Bandari ya Dar es Salaam, baada ya kubainika kuwa hazifai kwa matumizi ya binadamu.
Maofisa wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) wamelazimika kufanya msako mkali kwenye baadhi ya maduka ya dawa jijini Dar es Salaam baada ya kubainika kwamba tayari kondomu hizo zipo sokoni.
Akizungumza na waandishi wa habari jana Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Leandri Kinabo alizitaja kondomu hizo kuwa ni aina ya Melt Me zenye thamani ya Sh222.1   milioni zilizokamatwa tangu Oktoba 23 mwaka huu na kuzuiliwa bandarini hapo kwa taratibu zaidi za kisheria.
“Jambo lililotushtua ni kwamba zimebainika kwamba zipo madukani, tukajaribu kufuatilia tena bandarini tukifikiri kuwa huenda zimetolewa kinyemela licha ya kuzuiliwa ili ziteketezwe au zirejeshwe nchini India kwa gharama zao wahusika.
Tulipokwenda bandarini tukabaini kwamba bado zipo katika hali ile ile, kumbe  zimeingizwa nchini kwa njia ya panya, kwa kweli ni mbovu na ndiyo maana tumelazimika kuwajulisha wanahabari ili muwape taarifa wananchi wawe makini,” alisema Kinabo.
Alifafanua zaidi kwamba kondomu hizo ni mbovu kwani zimebainika kuwa na vitundu, pia zinapasuka haraka, hazina kabisa viwango vya ubora wa bidhaa unaotakiwa na Shirika la Viwango la Kimataifa (ISO).
Kinabo alisema kuwa TBS bado wanaendelea kufanya mawasiliano na kampuni iliyotengeneza kondomu hizo, lakini kwenye kasha  lake inaonyesha kuwa inaingizwa nchini na kampuni ya Fair Deal Exim ya Dar es Salaam.   

Katibu Bavicha Tanga ‘kukiona’

 
UONGOZI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) mkoani hapa, umeapa kumshughulikia ipasavyo Katibu wa Baraza la Vijana la chama hicho (Bavicha), mkoani Tanga, Deogratias Kisandu kwa kile kilichoelezwa kuwa ni utovu wa nidhamu.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mwenyekiti wa Chadema mkoani humo, Saidi Mbwete alisema kitendo cha Katibu huyo kumtaka Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Wilbrod Slaa ajiuzulu kwa kumiliki kadi ya CCM ni cha utovu wa nidhamu.
Mbwete alisema kauli na vitendo vya katibu huyo, vinaonyesha utovu wa nidhamu na kumdhalilisha Dk Slaa.
Alisema mtu anapohama chama kimoja na kujiunga na kingine, huwa amejitoa moja kwa moja kutoka kwenye chama chake cha awali.“Kurudisha kadi ya chama cha awali, ni hiari ya mwenye kumiliki kadi hiyo kwani ni yake kwa sababu ameinunua na kuilipia,” alisema Mbwete.
“Hata katiba za vyama vingi hazisemi kwamba mwanachama anapokihama chama chake, anatakiwa arudishe kadi,” alisisitiza
Mwenyekiti huyo alisema uongozi wa mkoa wa chama hicho, umekuwa ukifuatilia nyendo za kiongozi huyo wa Bavita na kugundua kuwa anatumiwa na CCM ili aivuruge Chadema.
“Tumegundua kuwa huyu si mwenzetu kwa sababu mawazo yake huwa kwake ni uamuzi ya kikao, ndiyo maana hata tangazo lake la kumkosoa Dk Slaa halikuwa na baraka za kikao,” alibainisha.
Hata hivyo, Mwenyekiti huyo alisisitiza kuwa wao kimkoa hawana mamlaka ya kumfukuza katika uongozi au uanachama isipokuwa watapeleka mapendekezo yao kwenye vikao vya ngazi ya juu kwa uamuzi wa mwisho.
Madai hayo ya kumshughulikia katibu huyo, yamekuja baada ya kutoa waraka unaomtaka Dk Slaa ajiuzulu kutokana na kumiliki kadi mbili za vyama vya siasa.

Na Raisa Said, Tanga

Most Popular Cities in 2012

Las Vegas

Las Vegas


 Chicago

 Chicago

 London

 London

 New York

 New York City

  Washington, D.C.

 Washington, D.C.

 San Francisco

 San Francisco

 San Diego

 San Diego

Dubai

 Dubai

New Orleans

 New Orleans

Hong Kong

 Hong Kong

COAST UNION YA TANGA YAPATA NAFASI YA PILI KOMBE LA UHAI


Azam mabingwa Kombe la Uhai 2012


 Wachezaji wa Azam wakishangilia baada ya kutwaa ubingwa wa Kombe la Uhai kwa kuifunga Coastal Union kwa penalti 3-1 jana kwenye Uwanja wa Karume. Picha na Michael Matemanga 


AZAM imenyakua ubingwa wa Kombe la Uhai kwa kuichapa Coastal Union kwa penalti 3-1, baada timu hizo kutoka sare 2-2 katika dakika 120 kwenye Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.
Shujaa wa Azam alikuwa kipa wao Aishi Manula aliyeokoa penalti tatu kati ya nne zilizopigwa na Coastal Union na kuipa ubingwa timu yake.
Kwa ushindi huo Azam wamejinyakulia kitita cha Sh1.5 milioni, Coastal Union wakiondoka Sh1 milioni, huku mabingwa wa msimu uliopita Simba wakiondoka na Sh500,000 kama washindi wa tatu.
Katika mchezo huo Azam walianza mchezo huo kwa kasi na kufanikiwa kupata bao la kuongoza katika dakika 11 kupitia, Samwel Mkomolo, kabla ya Kelvin Friday kupachika bao la pili kwa mkwaju wa penalti katika dakika 34.
Coastal Union ‘Wagosi Wakaya’ walibadilika kipindi cha pili na kufanikiwa kupata mabao ya kusawazisha yaliyofungwa kwa kichwa kwa kupitia Mohamed Miraji katika dakika 61 na Ally Iddi (77) na kufanya mchezo huo kwenye dakika 30 za nyongeza.
Fainali hiyo ilishudiwa na Rais wa TFF, Leodegar Tenga, Idd Kipingu na Said Mohamed mwenyekiti wa Azam pamoja na mamia ya mashabiki waliojitokeza kwenye uwanja huo.
Mshambuliaji wa Simba, Ramadhani Mzee alinyakua Sh300,000 tuzo ya ufungaji bora baada ya kufunga mabao sita, huku mchezaji bora wa mashindano, Joseph Kimwaga wa Azam alipata Sh350,000.
Ruvu Shooting ilitwaa tuzo ya timu yenye nidhamu itakabidhiwa Sh400,000, wakati kipa bora Mansour Ally wa Coastal Union alipata Sh300,000.
Kocha bora Bakari Shime wa Coastal Union alizawadiwa Sh300,000 kama ilivyokuwa kwa mwamuzi bora wa michuano hiyo.
AZAM imenyakua ubingwa wa Kombe la Uhai kwa kuichapa Coastal Union kwa penalti 3-1, baada timu hizo kutoka sare 2-2 katika dakika 120 kwenye Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.
Shujaa wa Azam alikuwa kipa wao Aishi Manula aliyeokoa penalti tatu kati ya nne zilizopigwa na Coastal Union na kuipa ubingwa timu yake.
Kwa ushindi huo Azam wamejinyakulia kitita cha Sh1.5 milioni, Coastal Union wakiondoka Sh1 milioni, huku mabingwa wa msimu uliopita Simba wakiondoka na Sh500,000 kama washindi wa tatu.
Katika mchezo huo Azam walianza mchezo huo kwa kasi na kufanikiwa kupata bao la kuongoza katika dakika 11 kupitia, Samwel Mkomolo, kabla ya Kelvin Friday kupachika bao la pili kwa mkwaju wa penalti katika dakika 34.
Coastal Union ‘Wagosi Wakaya’ walibadilika kipindi cha pili na kufanikiwa kupata mabao ya kusawazisha yaliyofungwa kwa kichwa kwa kupitia Mohamed Miraji katika dakika 61 na Ally Iddi (77) na kufanya mchezo huo kwenye dakika 30 za nyongeza.
Fainali hiyo ilishudiwa na Rais wa TFF, Leodegar Tenga, Idd Kipingu na Said Mohamed mwenyekiti wa Azam pamoja na mamia ya mashabiki waliojitokeza kwenye uwanja huo.
Mshambuliaji wa Simba, Ramadhani Mzee alinyakua Sh300,000 tuzo ya ufungaji bora baada ya kufunga mabao sita, huku mchezaji bora wa mashindano, Joseph Kimwaga wa Azam alipata Sh350,000.
Ruvu Shooting ilitwaa tuzo ya timu yenye nidhamu itakabidhiwa Sh400,000, wakati kipa bora Mansour Ally wa Coastal Union alipata Sh300,000.
Kocha bora Bakari Shime wa Coastal Union alizawadiwa Sh300,000 kama ilivyokuwa kwa mwamuzi bora wa michuano hiyo.