Thursday, February 14, 2013

Papa: Nimejiuzulu kwa hiyari

“Kama mnavyofahamu, nimeamua kuachia madaraka niliyopewa na Mungu Aprili 19, 2005,” alisema na kushangiliwa. Aliongeza: “Nimefanya hivi kwa uhuru kamili kwa manufaa ya kanisa.”
Alisema:

 Jumatatu wakati akitangaza kujiuzulu, baadhi ya makardinali waliokuwapo walibubujikwa machozi.
Kumekuwa na mawazo tofauti kuwa huenda uamuzi huo haukutokana na afya yake kuyumba wala umri wake mkubwa, bali huenda kuna shinikizo linalotokana na masuala mengine ama ya kihistoria au kisiasa.
Wachukunguzi wa masuala ya Kanisa Katoliki wanasema hata umri wa miaka 78 aliokuwa nao alipochaguliwa kuwa Papa mwaka 2005 tayari ulikuwa mkubwa na wakati huo hakikuonekana kikwazo.
Pia wanasema mbali na kuwa wapo mapapa wengine waliowahi kujiuzulu kabla, lakini suala hilo si la kawaida ndani ya kanisa, na halikuwahi kutokea kwa miaka 600 iliyopita, tangu alipojiuzulu Papa Gregory XII mwaka 1415.
Hata hivyo, Vatican imeendelea kushikilia kuwa sababu ya kujiuzulu kwa kiongozi huyo ni kulegalega kwa afya yake na umri mkubwa, huku ikithibitisha kuwa Benedict (Joseph Rutzinger) amefanyiwa upasuaji wa moyo miezi mitatu iliyopita.
Msemaji wa Vatican pia alikiri jana kuwa moyo wa Papa unasaidiwa na kifaa maalumu kinatumia betri inayochajiwa mara kwa mara.
-Ni uamuzi wa kustukiza sana ila kuna maana kubwa na tungependa pia kuifahamu.

JK awapa polisi ‘meno’ kudhibiti maandamano

“Wajibu wenu umetajwa kisheria, mamlaka yenu mlikabidhiwa na Bunge na wanapopiga kelele kuwa mmetumia nguvu kubwa, waambie sheria mmezitunga ninyi kwa hiyo nendeni mkazibadilishe,”

Aliwaagiza polisi kutimiza wajibu wao kuhakikisha wanadhibiti vurugu zote bila ya kusikiliza maneno ya wanasiasa na watu wengine, ambao wanalaumu bila  kujua kazi nzuri inayofanywa na askari.
“Wajibu wenu umetajwa kisheria, mamlaka yenu mlikabidhiwa na Bunge na wanapopiga kelele kuwa mmetumia nguvu kubwa, waambie sheria mmezitunga ninyi kwa hiyo nendeni mkazibadilishe,” alisema Rais Kikwete.
Pia, Rais Kikwete alishangazwa na  kauli za watu kuwa, polisi wanatumia nguvu kubwa kupita kiasi, lakini hajajua tafsiri hiyo inacholenga.
Aliwaagiza polisi kufanya kazi kwa uweledi na kujituma zaidi kulingana na mafunzo waliyoyapata kutoka vyuoni, ikiwamo  kutafuta jinsi bora ya kuzuia machafuko hata kabla ya kutokea.
Akitaja baadhi ya vyanzo vya vurugu hizo, alisema ni kutokana na baadhi ya wanasiasa kushindwa kutii maagizo ya polisi hata pale wanapozuiwa kufanya mikutano.
Awali, Mkuu wa Polisi nchini, Said Mwema alisema wanaendelea  kuratibu na kusimamia mikakati  kuhakikisha wanakuwa wa kisasa zaidi.