Tuesday, June 4, 2013

ENEO KUBWA KWA AJILI UFUFUAJI WA VIWANDA LATENGWA JIJINI TANGA

Na Benedict Liwenga-Maelezo, Dodoma.

Serikali kupitia Mamlaka ya EPZ imetenga eneo lenye ukubwa wa Hekta 1,363 katika Mkoa wa Tanga kwa ajili ya ujenzi wa viwanda na uthamini wa eneo husika umekamilika.

Hayo yamesemwa Bungeni Jijini Dodoma wakati Waziri wa Uwekezaji, Mhe. Mary Nagu akijibu swali la Mhe. Omari Rashidi Nundu kwa niaba ya Waziri wa Viwanda na Biashara aliyetaka kujua ni matayarisho na utekelezaji upi unafanywa na Serikali  uweza kutekeleza azma hiyo katika kipindi cha mwaka 2010-2015 na ni nini hatma ya Viwanda vya zamani ambavyo kwa muda mrefu havifanyi kazi.
 Mhe. Nagu amesema kuwa mkakati wa kuufanya Mkoa wa Tanga kuwa jiji la viwanda upo katika hatua nzuri na kuongeza kuwa kwa hivi sasa viwanda vipya vilivyojengwa na vinavyojengwa ni pamoja na kiwanda cha NILCANT cha kutengeza chokaa, kiwanda cha Rhino Cement pamoja na kiwanda cha Sungura Cement ambacho kinatarajiwa kujengwa.
“Jiji la Tanga limeingia ubia na kampuni ya Korea (GoodPM) kwa ajili ya kutekeleza mradi mkubwa wa kujenga viwanda 15 katika eneo la ekari 73 huko Pongwe unaotarajiwa kuanza mwezi Mei mwaka huu chini ya utaratibu wa Tanga Economic Corridor”. Alisema Waziri Nagu.
Akijibu swali la nyongeza toka kwa Mhe. Nundu lililotaka kujua kama Serikali iko tayari kufanya tathmini kufufua viwanda vya zamani, Waziri Nagu amesema kuwa Serikali inakubaliana na hilo na iko tayari kuhakikisha viwanda hivyo vinafufuliwa.
 Aidha Mhe. Nagu aliongeza kuwa Serikali ni moja hivyo itashirikiana na Wizara ya Viwanda kupitia Waziri wa Viwanda kuhakikisha kuwa viwanda vya zamani vinafufuliwa.

Tuesday, April 2, 2013

Kikwete: Sibagui dini yoyote nchini

 http://www.mwananchi.co.tz/image/view/-/1736606/highRes/484917/-/maxw/600/-/elgirl/-/jk.jpg
Rais Jakaya Mrisho Kikwete

Rais Kikwete alisema hayo juzi katika hotuba yake ya ambayo huisoma kila mwishoni mwa mwezi, kauli ambayo imekuja wakati kukiwa na malalamiko kwamba Serikali imekuwa ikifumbia macho matukio ya uhalifu wenye sura ya uhasama wa kidini.

“Mimi binafsi sibagui, hushiriki shughuli za Waislamu na Wakristo kila ninapoalikwa labda nikose nafasi kwa sababu nyinginezo,” aliongeza Rais Kikwete.

Alisema kuna baadhi ya watu wamekuwa wakisema nchi inaendeshwa kwa mfumo wa Kikristo na kwamba amekuwa akipendelea kushiriki zaidi katika shughuli za Kikristo kuliko za Waislamu.
“Naambiwa kuwa niko mwepesi kushiriki maziko ya maaskofu kuliko ya masheikh wanapofariki.

“Kuna misikiti mitatu ya Jijini Dar es Salaam ambayo iliwahi kunisomea itikafu ili nife kwa sababu za kubagua dini yao.
“Katika itikafu hiyo waliwajumuisha Inspekta Jenerali wa Polisi, Said Mwema na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova,” alieleza Kikwete.
“Nimeshashiriki mazishi ya Masheikh kama nifanyavyo kwa maaskofu na watu mbalimbali Waislamu na Wakristo,” alisema.

Alifafanua pale ambapo hakushiriki mazishi ya sheikh au askofu itakuwa ni kwa sababu ya kubanwa na shughuli nyingine ambazo ni lazima zifanywe na yeye au taarifa ilikuwa ya muda mfupi.
“Waislamu desturi yetu ni kuzika mara mtu anapofariki, hicho ni kikwazo kwangu kushiriki mazishi ya masheikh hasa ikiwa ni nje ya Dar es Salaam kwa sababu ya taratibu za kumsafirisha Rais kutoka mahali pamoja kwenda pengine siyo nyepesi,” alisema Kikwete.

Alisema pia Waislamu wanadai kuwa kitabu chao kitakatifu, yaani Quran Tukufu, kinadhalilishwa kwa kuchanwa, kuchomwa moto na kukojolewa na Wakristo na Serikali haichukui hatua yoyote ya maana. Alisema imefika mahali viongozi na waumini wa dini hizo kubwa mbili kama hawatakubali kubadili mwelekeo wa sasa basi tunakoelekea ni kubaya
“Nchi yetu tutaivuruga na sifa yake ya miaka mingi ya Waislamu na Wakristo kuishi pamoja kama ndugu itatoweka. Tanzania itaacha kuwa kisiwa cha amani na kuingia katika orodha ya nchi zenye migogoro na hata vita ya wenyewe kwa wenyewe,” alisema Kikwete.

Alisema Serikali haifurahishwi na kitendo cha mtu kudhalilisha dini ya mwenzake ndiyo maana wapo wahadhiri wa dini ya Kiislamu na wahubiri wa dini ya Kikristo ambao wamekamatwa na kufunguliwa mashtaka katika matukio tofauti.
“Vyombo vya usalama vinatambua wajibu wao na kama havitimizi wajibu wao huo utakuwa ulegevu wao na siyo kwamba ni sera na maelekezo yangu au ya Serikali,” alisema Kikwete.

Aliongeza; “Mtakumbuka kuwa mara kadhaa nimewakumbusha wakuu wa mikoa, wilaya na vyombo vya usalama kuacha ajizi katika kutimiza wajibu wao kwenye suala hili.”

Kikwete alisema kuuawa kwa viongozi wa dini na kuchomwa makanisa kusichukuliwe kama Serikali yake imeshindwa kulinda usalama wa raia wake.

“Kama ingekuwa hivyo, tungeshuhudia mauaji ya raia, viongozi wa dini na matukio ya kuchomwa nyumba za ibada yakiwa mengi hapa nchini,” alisema Rais Kikwete.

Ajali ya Jengo la ghorofa lililoanguka

Kikwete alisema sheria zitafuata mkondo kwa waliosababisha kuanguka kwa jengo hilo baada ya uchunguzi unaofanywa na Bodi ya Usajili wa Wahandisi.

Alisema watakaobainika kuhusika watatakiwa kufikishwa mahakamani ikiwa ni pamoja na kufutiwa leseni zao za kuendesha shughuli za ujenzi.

Alitaka mikoa yote nchini kujifunza katika ajali hiyo kwa kufuata kanuni za ujenzi ili kuondokana na maafa yanayoweza kujitokeza.

Monday, April 1, 2013

Ajali; Simulizi ya aliyenusurika kifo kutoka ghorofa ya 15


Rais Kikwete na Mkewe, Mama Salma Kikwete wakimpa pole Yusuph Abdallah katika Hospitali ya Muhimbili walipotembelea majeruhi wa ajali ya kuporomoka jengo la ghorofa 16

“Majira ya asubuhi kati ya saa mbili na saa tatu hivi nilipokea simu kutoka kwa rafiki yangu jina maarufu anajulikana kama Tafu, ambapo alinitaka niende nikaonane na mkandarasi wa jengo hilo ili anipe kazi ya kuweka madirisha,” anasema Mlela.
Anasema wakati akijiandaa kutoka mke wake alimwambia siku hiyo apumzike asiende kufanya kazi naye akakubali, lakini haikupita muda mrefu mke wake alimfuata na kumuuliza amesikia taarifa kwamba kuna jengo limedondoka?
“Niliamua kwenda katika eneo la tukio na ndipo alipogundua kwamba eneo hilo ndiyo alipotakiwa kwenda kufanya kazi. Wakati juhudi za uokoaji zikiendelea nilijaribu tena kumpigia simu rafiki yangu.Nikiwa bado kwenye eneo la tukio ghafla nikaona mguu ukitolewa kwenye mchanga na nilitambua ulikuwa mguu wa rafiki yangu baada ya kuona kiatu chake.”

Sunday, March 31, 2013

mtaa wa Indira Ghandi jijini Dar es salaam

jengo lililoporomoka na shughuli za uokozi mtaa wa Indira Ghandi jijini Dar es salaam Machi 29, 2013

PICHA TOFAUTITOFAUTI ZIKIONESHA SHUGHULI ZA UOKOZI ZINAVYOENDELEA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjih22Xpq4njTzY8r3PphRh1uZLSdgFIef-WoxGAMpYdIWWVJpPAkIqdPOMIE6Iosu6bIhMmr6VTHXaFxU0YS2bs3BNF9NLYmkkGWpTsKzdx95fxVx4NGxofEamb9i8G8suruGPCMa5UT4/s1600/Untitled.png



https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiDNt_J7aN8oKOA8LqIXNxm_JK54Hpek10yREe0fWr8B3znTOKOn3js8zr0yU1FT-a0u3D5ZCRABZtgcKMM3bmTf2NzPXSGerNYjqv_Py4k8nR5uXs6VCy6gBEWiQuSR9_MhC0FNJaLLZw/s1600/GOPR5667.jpg

 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjV3mdlwf41pkcC97srIC_03kq8upqudKc5mZD29C2V5F1XaKhK1KeLZYYTOYX6Eus92mYrgpy5chiFcayDibPgwZoj9qcXEl7X13f975a2qo46qVRuJ4wwh-JFaT-cilhmqZPNSnVLvdg/s1600/GOPR2834.jpg

 
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiEVkc1EdrBnnEqFbPH3MUbkUtPEs-9ijULF3EwYVrQvf28oY8a1pocmmmj3VL-bosbM4jEy0M2C9unnh535L2diJakEJ3MwqJXyRmGJJ09Df5kN7hiCBHSOSg3mPN28jnP77iir_W3EOQ/s1600/C27B5717.jpg

Wednesday, March 27, 2013

ibada takatifu ya kubariki mafuta ya Krisma na kurudiwa kwa kiapo cha mapadri, iliyofanyika katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Joseph, jana.

http://www.mwananchi.co.tz/image/view/-/1731754/highRes/482598/-/maxw/600/-/dhe7iaz/-/pengo.jpg
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Kanisa Katoliki la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, akiendesha ibada takatifu ya kubariki mafuta ya Krisma na kurudiwa kwa kiapo cha mapadri, iliyofanyika katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Joseph, jana. Picha na Emmanuel Herman.


Kiongozi wa Kanisa  Katoliki nchini, Mwadhama Kardinali Polycarp Pengo, amewataka mapadri wa Kanisa hilo kuwa kioo kwa matendo mema kwa kila wanachokifanya kwa wengine.
Kardinali Pengo aliyasema hayo jana wakati wa misa ya sherehe ya Sakramenti ya Upadri na kubariki mafuta ya Pasaka katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Joseph jijini humo.
Alisema ni lazima kuwa watimilifu wa kibinadamu kwa kupitia njia ya sadaka, mateso na kifo hivyo kuwataka kuwafundisha yaliyo mema na yenye kumpendeza Yesu Kristu.
“Ili kufikia ukamilifu hatuwezi kukwepa misalaba, waumini mnatakiwa kutuombea ili kuweza kumwakilisha Yesu Kristu kwa matendo yaliyo mema na ya kumpendeza,” alisema Kardinali Pengo. “Hivi sasa  shida na mahangaiko ya dunia ni mengi  lazima  kumwonyesha Yesu ili aweze kutusadia na kushinda.
“Tukianza kuangalia chanzo cha matatizo na mahangaiko yalivyo hivi sasa hatuwezi kufika na tutaangamia,” alisema Kardinali Pengo.
Alisema njia nyingine zozote ambazo zinashabikia kama anasa na ukatili haziwezi kufanikiwa, hivyo aliwataka Mapadri hao kuwahubiria amani waumini.

Tuesday, March 26, 2013

MAFUNZO YA MGAMBO JKT YAMEFUNGWA RASMI LEO

 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjRngLz7DOBnW22i2cxjGzU3nqIck3t1bYybkRgD55xIXTRMQKp35LXrLLkl4asSJJIhgepUFLGgCExABtjia3OshhMEW3A7qPWhQtI8wUG2Eqa1r4bBsFcclCWyuHfxZjk6xAxAehm21g/s1600/8E9U3088.JPG
Mheshimiwa Esther Bulaya akikabidhiwa cheti cha kuhitimu mafunzo ya mgambo RUVU JKT na Amiri jeshi mkuu wa Tanzania,Raisi wa Jamhuri ya Muungano Jakaya Mrisho Kikwete

 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgdt0nvR_tBWIXPePxX5qfj1-l6ABcDVNgYPd0L8qvTxxJQN1LtOONhJu-qi94zKesrM-b2lRezcFbDK1IfjjQaYaIh9rc1lVqlDhjQ9fq4TGIfsAmqu4bDiCjAhwQ5eaJioDH8k5xZn-k/s1600/9.JPG
Mheshimiwa Zitto Kabwe akikabidhiwa cheti cha kuhitimu mafunzo ya mgambo MGAMBO JKT Wilaya ya Handeni na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tanga,ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Handeni Muhingo Rweyemamu


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEha0ZSoXAUq10TBbx-rMFAE1JdhvB3uIjHv7EDcv0nJTSSfzvylBFih9kvD9nsSGAlDzPxRd7bq19Ru8O2SiyWq0YP_9csqOIBlwweXJcHPkWN0YU8LZRWMCWKFjeXmNA6CXm7OOlL4Q80/s1600/8E9U3018.JPG
Baadhi ya Waheshimiwa wakila kiapo,kushooto ni Halima Mdee


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiu9us9yJS57IAlllZNSKWZnzJgd3G1GJPEgLvl1Fv2qdKabnRnyQh-Mvc-FBgDgYZXcL4zqQUoDlA0uDpUmw8lDajB-JwwgvqyJff6SPfz_TMqJ9IW4sNCkr8N20HPKThhOmqXkGp85xE/s1600/1+(2).JPG
Upande wa mbele kushoto katikati ni Iddi Azani akihitimu mafunzo ya mgambo na wenzake kwa kutembea kwa ukakamavu


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiF4cZ6TxpgJC4BNaBwaTUfvi_oGoH3L3Ek_ML735mBrFyzlQXzjMtWURXq6IXAMRLiS8A_TrB4SagEmLu6F2WKanfbfCHnaE1PbQA-lnDQ2KXmknrGTJ8qh77jzbo-QWzHh4E4-Gh5b5I/s1600/5.JPG
Mbunge Athanas Mbassa wa Biharamulo akila kiapo Kambi ya Mgambo JKT Tanga


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjxmRjQeCKnETW0w-XkIuW46C4v7RaPT9PnH4_achfRrj6GP1fTvJwqydCdZwY7KCrhm42FqIj2t7QnE_0JgGEQFkthZI6ThhoB-GD_gD8nTfWLfiiA7FWIektcrU9zqBq1wKe7oe0gDxI/s1600/6.JPG
Mheshimiwa Abdallah Hjji Alli,Mbunge wa Kiwani Pemba akihitimu mafunzo ya Mgambo JKT Tanga

 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh-wTNwREgx-fHGjKgLMNRC3BgY5KcohGedz7-k45s6hk0z4UN0SlLCShPUDQF8iGaO90QBtK2XiIqCmT_nIuO3xGI_J3MHA9LUMAs804dR3suJ7VSh-XcyRRRsXIwHihOurwbqUpIWufA/s1600/7.JPG
Mbunge Raya Khamisi wa Viti Maalumu naye alihitimu mafunzo ya Mgambo JKT Tanga

 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg1DqPzMobpATbfQFBdxJ4cxSKCS8r4ec6v2JuXvxuMFXka2aPppnFqnamtQW3iyxeQzQj8WciC-crNDsFeq7ECpaSx08ryYm5TN3Zn3nzBsy28X4XTQNKhqyiZ4QnzibY_9mCHbnLlQVI/s1600/8E9U3151.JPG
 Mbunge wa Mtera Mheshimiwa Livingstone Lusinde *kibajaji* alihitimu mafunzo(watatu kutoka kulia)

Monday, March 11, 2013

tanzania hatarini kufungiwa fifa


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiB8e3u-phmmb0iOw8ItXTaj-ZQeRQc-AEgxcMyp4R4JRqRZfjwIYXwdpXb1mWu_SyxHInz3y0cdmxyEqITamhnIwQUK7Qn8QxNfFFtSgWot4lP_aSizNpepOuKJsucWp5w8PPlWLWxJcM/s1600/1-fifa-logo.jpg
SHIRIKISHO LA SOKA

OFISA Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniface Wambura 
--
Shirikisho la Kimataifa la Vyama vya Mpira wa Miguu (FIFA) limesema litaifungia Tanzania iwapo itabainika kuwa Serikali imekuwa ikiingilia shughuli za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

FIFA imesema kumekuwa na shutuma kupitia taarifa mbalimbali za vyombo vya habari nchini kuwa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo imeonesha nia ya kuingilia uendeshaji wa TFF.


Kwa mujibu wa barua ya jana (Machi 10 mwaka huu) ya FIFA kwenda kwa Rais wa TFF, Leodegar Tenga, vyombo vya habari vimemkariri Waziri (Dk. Fenella Mukangara) kuwa Serikali imeiagiza TFF kutumia Katiba ya mwaka 2006 katika uchaguzi wakati tayari imeshafanyiwa marekebisho.

“Pia imeelezwa kuwa TFF imetakiwa kufanya Mkutano Mkuu pamoja na ule
wa uchaguzi kwa tarehe ambazo zimepangwa na Serikali. Vilevile imeelezwa kuwa Serikali inakusudia kuunda Kamati ya Muda iwapo TFF haitatekeleza maagizo yake,” imesema sehemu ya barua hiyo iliyosainiwa na Katibu Mkuu wa FIFA, Jerome Valke.

FIFA imesema iwapo yaliyoripotiwa na vyombo vya habari yatathibitika kuwa kweli, maana yake huo ni uingiliaji wa wazi wa Serikali kwa shughuli za TFF.

“Tunapenda kuwakumbusha kuwa wanachama wote wa FIFA wanatakiwa kuendesha shughulizao kwa uhuru bila kuingiliwa na mtu mwingine kama ilivyoelezwa katika ibara za 13 na 17 za Katiba ya FIFA.

“Hivyo kama maagizo hayo yanayodaiwa kutolewa na Serikali yatatekelezwa, suala hili litapelekwa katika mamlaka za juu za FIFA kwa hatua zaidi ikiwemo  kuisimamisha Tanzania kama ambavyo inakuwapale panapokuwa na uingiliaji wa Serikali,” imesema barua hiyo.

Barua hiyo ambayo nakala yake pia imetumwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) imeelezea baadhi ya athari ambazo Tanzania itakumbana nazo endapo itasimamishwa ni timu za taifa pamoja na klabu kutoshiriki mechi za kimataifa kwa mujibu wa Ibara ya 14 ya Katiba ya FIFA.

Vilevile si TFF au wanachama wake na maofisa wengine watakaoweza kunufaika na programu za maendeleo, kozi au mafunzo yanayotolewa na FIFA na CAF.

“Madai ya uamuzi uliofanywa na Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo ni ya kusikitisha kutokana na ukweli kuwa FIFA ilishatangaza itatuma ujumbe wake kuchunguza jinsi hali ilivyo kwa sasa na kutoa mapendekezo yake. Kutokana na hali hii, ujumbe wa FIFA uliokuwa uje kuchunguza(suala la uchaguzi) itabidi usubiri kwa vile ni muhimu kushughulikia tatizo hili kwanza.

“Katika mazingira haya tunaomba ueleze msimamo huu wa FIFA kwa mamlaka zinazohusika (Serikali) na athari ambazo mpira wa miguu wa Tanzania utakumbana nazo. Tunakushuru na tunatarajia utatufahamisha kila hatua inayoendelea katika suala hili,” imesema barua hiyo.

OFISA Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF),
Boniface Wambura

Saturday, March 9, 2013

vigogo wavuliwa madaraka TBS

Profesa Mhilu alisema hatua hiyo imekuja baada ya bodi hiyo kufanya usaili kwa vigogo mbalimbali wa shirika hilo
http://www.mwananchi.co.tz/image/view/-/1714304/highRes/473595/-/maxw/600/-/no9v67z/-/tbss.jpg'

 Profesa Mhilu alisema hatua hiyo imekuja baada ya bodi hiyo kufanya usaili kwa vigogo mbalimbali wa shirika hilo,Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Profesa Cuthbert Mhilu alisema jana kuwa waliovuliwa madaraka ni aliyekuwa Mkurugenzi wa Udhibiti Ubora, Dominic Mwakangale na aliyekuwa Mkurugenzi wa Upimaji na Huduma za Vifungashio, Kezia Mbwambo.
 Baada ya hatua hiyo, bodi hiyo ilimteua Tumaini Mtitu kuwa Mkurugenzi mpya wa Udhibiti Ubora na Agnes Mneney kuwa Mkurugenzi wa Upimaji na Huduma za Vifungashio,Wengine walioteuliwa ni Emmanuel Ntelya atakayekuwa Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Shirika na Edna Ndumbaro kuwa Meneja Uandaaji Viwango vya Uhandisi.
Kadhalika, Matrida Kasanga ameteuliwa kuwa Meneja wa Hati na Tehama na Anitha Kaveva anakuwa Meneja Mipango na Utawala.
Alipoulizwa kama hatua hiyo inakwenda sanjari na sifa baada ya kufanyika kwa usaili Profesa Mhilu alisema: “Ninachowaambia ni hicho... hakuna tatizo tulilobaini kuhusu viongozi hawa, haya ni mabadiliko ya kawaida.”
Alipoulizwa kuhusu hatua hiyo, Mbwambo alijibu kwa kifupi: “Sifahamu, wasiliana na mwenyekiti wa bodi au  mkurugenzi mkuu ndiyo wenye nafasi ya kuzungumzia zaidi kuhusu hatua hiyo.”
Akizungumzia uteuzi huo, Profesa Mhilu alisema: “Hata hawa tuliowateua kushika nyadhifa hizo watambue kwamba tutawafuatilia kwa karibu tukiangalia utendaji wao, asiyefanya kazi kwa ufanisi atang’olewa.”
Alisema Bodi hiyo imetoa maagizo kwa Menejimenti ya TBS kuhakikisha kwamba inakomesha bidhaa feki, inafanya ukaguzi wa magari, pia kuhakikisha inaondoa urasimu wa upatikanaji wa leseni kwa wajasiriamali wadogo lakini kwa kuzingatia viwango vya bidhaa wanazotengeneza.
Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Joseph Masikitiko alisema kuwa amejipanga kushirikiana na menejimenti yake ikiwa ni pamoja na kukomesha makundi miongoni mwa wafanyakazi ili kuleta tija.
Tangu ilipozinduliwa, bodi hiyo imekuwa ikifanya kazi kubwa ya kusafisha safu za utawala za shirika hilo baada ya kuanza kwa kumvua madaraka Kaimu Mkurugenzi Mkuu Leandiri Kinabo na kumteua Masikitiko kabla ya kuitisha usaili upya wa wakurugenzi.

Friday, March 8, 2013

SAI BABA,basi linalofanya safari zake kutoka Ruvuma(kwa wakunyumba) kwenda Dar es salaam,limemgonga mwendesha pikipiki na kusababisha mauti yake



Hili ndilo basi lililomgonga  mwendesha pikipiki,lenye namba za usajili T 690 BUW.


Upande wa mbele wa basi lilipogongana


Abiria wakieleza ajali ilivyotokea eneo la Mburushi


 
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma Bw. Deusdedit Nsimeki alie vua kofia akiwa katika eneo la tukio maeneo ya kwa Mburushi


 
Pikipiki ya marehemu  Steven Adam (62) yenye namba za usajili  T 618 ATX

 

  Umati wa wasafiri wakiwemo wapita njia wakiangalia ajali hiyo mbaya iliyotokea leo majira ya saa moja asubuhi.

 Marehem Steven alikuwa ni mfanyabiashara,mkazi wa Liumbu Mletele akielekea mjini kupeleka maziwa yake kwa wateja ndipo alipopatwa na mauti hayo.Kwa maelezo ya wasafiri wamesema mwenye makosa ni dereva wa pikipiki ambaye hakuwa makini barabari kwa kuendesha vibaya na kwa mwendo kasi pasipo kuzingatia sheria za barabarani.

Wednesday, March 6, 2013

Ofisa elimu awavua madaraka walimu 50


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjuCV9LyT-zhZFca_QDGQlRo9uMbdItAY9KdhW35_-VI-6yhGZ4njzDmAneWU72KyR_lzgFFEyWW3qZ8klrk9EzvZPLbdzqpmQZJzquBoB-526v3fi9lvIW4DNR3L5Rjq22qsvFmQy7AiU/s1600/HakiElimu2.JPG

Kilindi. Ofisa Elimu ya Msingi Wilaya ya Kilindi, Mkoa wa Tanga, Geofrey Abayo amewavua madaraka walimu wakuu 50 wa shule za msingi, lengo likiwa ni kusuka upya timu ya kuinua kiwango cha taaluma.
Abayo aliamua kuchukua uamuzi huo baada ya matokeo ya darasa la saba mwaka jana wilayani hapa kuwa mabaya, baada ya asilimia 18 ya wanafunzi waliofanya mtihani ndiyo waliofaulu kujiunga kidato cha kwanza.
Alitoa taarifa hiyo mwishoni mwa wiki iliyopita kwenye mkutano na walimu wa shule za msingi na sekondari, uliofanyika katika kata tano za Kwediboma, Mabaranga, Negero, Kikunde na Songe.
Ofisa huyo akiwa ameambatana na Mkuu wa wilaya hiyo, Suleiman Liwowa  na Katibu Tawala Msaidizi Elimu Mkoa wa Tanga, Ramadhani Chomola walisema  walitarajia kupata matokeo hayo.
Alisema walitarajia watoto wengi kushindwa kutokana na kuongeza udhibiti katika usimamizi wa mitihani kitaifa kwa darasa la saba, kwa kuziba mianya inayotumiwa na baadhi ya walimu wasio waaminifu kuwapa majibu watahiniwa.
Abayo aliapa kuendelea kuwa mkali kwa walimu wanaowafanyia mitihani watoto ili wafaulu.
Mwalimu Ali Mganga wa Shule ya Msingi Kikunde, alipendekeza mitihani ya kitaifa ikishafanywa ipelekwe shuleni ili wanafunzi na walimu waweze kutambua walipojikwaa.
Hata hivyo, Mwalimu Mganga alitupia lawama kwa watungaji mitihani ya taifa  kwamba, haieleweki hivyo inachangia kwa kiwango kikubwa kufeli kwa watoto.
Naye Mwalimu Bakari Mwaliko wa Shule ya Msingi Mabaranga, Tarafa ya Mswaki, alishauri Serikali kuwachunguza watu waliosahihisha mitihani ya wanafunzi wa msingi na sekondari, akihisi huenda kuna hujuma za kisiasa.

Wednesday, February 27, 2013

SHULE TOFAUTI ZA SEKONDARI NA MAZINGIRA YAKE

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjfjQpM09Na70fzoUWHeslwmP5WTgujkgGaogY7-GyphHtucDAJXR7_bfzV7NjF7JWav5yXDFikF4jfxbC105bD4SENC5raRFqw6nP_Geb5ukLEYGR5uj86F019lgWVA1SanQpY_6vveG4/s1600/r2.png
MTWARA:MASASI SEC

 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjilULZGgCgcrh1AoUfSGi6vO9o1xN_h7SgRTGe4UMpajQbd5ozVo8ZUhFDcKlupiDBgkDjkXJQKL6TtnjnV_gR29URTZeykUqo5Kq1CJLeKNMVDzxvPLqb1EzJZOK0SSn7vPCIYrAcXak/s1600/r5.pngLINDI:NGONGO SEC

 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi474uKMA56V0_sDTFbqCnl25Jy57jTq_ukmizQfBfunmAaSwxGyJgEZ4gAjecKXPJdh_VfthpHoGAT-re8tMvMIYRXQ408N3vvvWAisPRjXF76Dm-D3FsT9WBvtoN-M4P3OcKUOgUaJKU/s1600/r4.png
MOROGORO:MANDELA SEC


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjRHs4nerjKiNpme8-IryhLhioFKG7tMVtThdWt6T3hhua6csStr9erWUDKfoBw8FaxdWo5mbfAzBVoRc4wBI1pVODLNyog9r0Ss5eZagxY4s3ftDG7LnjSBEpK2AWrhLRniuklZfUO6wY/s1600/r6.pngDAR ES SALAAM:TWIGA SEC

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiB4_nE9rW2huuIjuwn8bqvameeJ88Vvosw3Cyw6KoQw8g9tr-5SRbhccPxz-FiFiEssq_rc4yhgEK06Qtv2_ZY7yUj7q8fc2_rqpWiRC4SARzcRxmPeFqHKesART9iJl2licB9_cic9vU/s1600/r3.png
PWANI:KISARAWE LUTHERAN SEMINARY

Urais 2015: Utafiti wa Synovate wapondwa,wadau wadai una ajenda ya siri

 
Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba ambaye amesema haziamini tafiti zinazotolewa na Syonovate akidai hazina ukweli wowote.


Katika maoni yao, baadhi ya wasomi kutoka taasisi mbalimbali za elimu ya juu nchini walieleza wasiwasi wao kuhusu usahihi wa matokeo hayo na kuhoji mbinu zilizotumika wakisema inawezekana hazikuwa sahihi.
Mhadhiri wa Sayansi ya Siasa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Alexander Makulilo ameuponda akisema haukufuata misingi ya sayansi ya siasa.
Dk Makulilo alisema alifanya utafiti kwa kampuni zinazofanya tafiti kama hizo kati ya mwaka 2010 hadi 2011 na kugundua udhaifu mkubwa katika kampuni hizo.
“Kwanza wanakosea, kwa mfano wanaposema kuwa utafiti huu ni mwendelezo wa ule uliofanyika Desemba 5 hadi 18, 2011. Ukichunguza utakuta data hizo hazipo. Zilizopo ni za Mei 2 hadi 19, 2011.”
“Kwa kawaida uelewa wa wananchi wa vijijini ni mdogo ukilinganisha na mijini kwa sababu mijini kuna vyombo vya habari. Kwa mfano, ukiangalia swali la nani anafaa kuwa Rais, mwaka 2011 walisema Dk Wilbrod Slaa alikuwa na asilimia 42, lakini sasa ana asilimia 17.
Vijijini wengi bado wanaikubali CCM kutokana na uelewa mdogo, iweje Dk Slaa ambaye chama chake hakina wafuasi wengi vijijini ashinde?” alihoji.
“Utafiti wa Synovate una dosari kubwa kisayansi, hauonyeshi tarehe wala wapi umefanyika. Waliohojiwa wameonyeshwa umri wao, lakini hawaelezwi maoni yao kulingana na umri, jinsia, wanatoka vijijini na mijini. Nilipofanya utafiti wangu niliwafuata wakakimbia…” alisema Dk Makulilo.
Mhadhiri mwingine wa UDSM, Profesa Gaudence Mpangala alisema nyakati za kuelekea Uchaguzi Mkuu, tafiti nyingi hufanyika zikiwa na malengo ya kubeba watu au chama fulani.
Hata hivyo, alisema kilichofanywa na Synovate ni utafiti hivyo kwa kuwa yeye hajafanya utafiti ni vigumu kuupinga moja kwa moja... “Ila kwa mtizamo wa kawaida unatia shaka.”

Thursday, February 14, 2013

Papa: Nimejiuzulu kwa hiyari

“Kama mnavyofahamu, nimeamua kuachia madaraka niliyopewa na Mungu Aprili 19, 2005,” alisema na kushangiliwa. Aliongeza: “Nimefanya hivi kwa uhuru kamili kwa manufaa ya kanisa.”
Alisema:

 Jumatatu wakati akitangaza kujiuzulu, baadhi ya makardinali waliokuwapo walibubujikwa machozi.
Kumekuwa na mawazo tofauti kuwa huenda uamuzi huo haukutokana na afya yake kuyumba wala umri wake mkubwa, bali huenda kuna shinikizo linalotokana na masuala mengine ama ya kihistoria au kisiasa.
Wachukunguzi wa masuala ya Kanisa Katoliki wanasema hata umri wa miaka 78 aliokuwa nao alipochaguliwa kuwa Papa mwaka 2005 tayari ulikuwa mkubwa na wakati huo hakikuonekana kikwazo.
Pia wanasema mbali na kuwa wapo mapapa wengine waliowahi kujiuzulu kabla, lakini suala hilo si la kawaida ndani ya kanisa, na halikuwahi kutokea kwa miaka 600 iliyopita, tangu alipojiuzulu Papa Gregory XII mwaka 1415.
Hata hivyo, Vatican imeendelea kushikilia kuwa sababu ya kujiuzulu kwa kiongozi huyo ni kulegalega kwa afya yake na umri mkubwa, huku ikithibitisha kuwa Benedict (Joseph Rutzinger) amefanyiwa upasuaji wa moyo miezi mitatu iliyopita.
Msemaji wa Vatican pia alikiri jana kuwa moyo wa Papa unasaidiwa na kifaa maalumu kinatumia betri inayochajiwa mara kwa mara.
-Ni uamuzi wa kustukiza sana ila kuna maana kubwa na tungependa pia kuifahamu.

JK awapa polisi ‘meno’ kudhibiti maandamano

“Wajibu wenu umetajwa kisheria, mamlaka yenu mlikabidhiwa na Bunge na wanapopiga kelele kuwa mmetumia nguvu kubwa, waambie sheria mmezitunga ninyi kwa hiyo nendeni mkazibadilishe,”

Aliwaagiza polisi kutimiza wajibu wao kuhakikisha wanadhibiti vurugu zote bila ya kusikiliza maneno ya wanasiasa na watu wengine, ambao wanalaumu bila  kujua kazi nzuri inayofanywa na askari.
“Wajibu wenu umetajwa kisheria, mamlaka yenu mlikabidhiwa na Bunge na wanapopiga kelele kuwa mmetumia nguvu kubwa, waambie sheria mmezitunga ninyi kwa hiyo nendeni mkazibadilishe,” alisema Rais Kikwete.
Pia, Rais Kikwete alishangazwa na  kauli za watu kuwa, polisi wanatumia nguvu kubwa kupita kiasi, lakini hajajua tafsiri hiyo inacholenga.
Aliwaagiza polisi kufanya kazi kwa uweledi na kujituma zaidi kulingana na mafunzo waliyoyapata kutoka vyuoni, ikiwamo  kutafuta jinsi bora ya kuzuia machafuko hata kabla ya kutokea.
Akitaja baadhi ya vyanzo vya vurugu hizo, alisema ni kutokana na baadhi ya wanasiasa kushindwa kutii maagizo ya polisi hata pale wanapozuiwa kufanya mikutano.
Awali, Mkuu wa Polisi nchini, Said Mwema alisema wanaendelea  kuratibu na kusimamia mikakati  kuhakikisha wanakuwa wa kisasa zaidi.

Tuesday, February 5, 2013

elimu yetu inavyojenga matabaka katika jamii.


 wanafunzi wa shule ya msingi wakiwa darasani,hii ndio tofauti kubwa kati ya shule yenye kutoa maarifa na ujuzi na shule yenye kutoa vyeti na sifa za kumuwezesha mtu kupata kazi.


MATOKEO mazuri au mabaya  ya elimu kwa mtu,  huonekana katika namna anavyotenda mambo na dhamira yake ya kutenda,  na wala hayatokani na alichojifunza, namna alivojifunza na sababu ya kujifunza.
Hiyo ndio tofauti kubwa kati ya shule yenye kutoa maarifa na ujuzi na shule yenye kutoa vyeti na sifa za kumuwezesha mtu kupata kazi.
Watu wengine wanapozungumzia elimu wanafikiri kuhusu utaratibu mzima wa kujifunza wenye lengo la kumpatia mtu ujuzi na maarifa na kumudu vyema kile alichojifunza.
Ujuzi na maaarifa ndio hasa lengo na upatikanaji wake  unaotarajiwa utumike katika kupambana na changamoto na hata kuibua na kuleta maarifa mengine zaidi.
Kuna watu wengine wanapozungumzia elimu,  wanafikiria umiliki wa cheti kinachoonyesha una ujuzi fulani.
Elimu ya aina hii sio kwa ajili ya kutumika katika maisha wala kutafuta maarifa mengine,  bali ni kwa ajili ya mtu kukariri anachojifunza na  kuyatoa yale maarifa yaliyokaririwa katika mitihani ili apate cheti kizuri kitakachowezesha kupata kazi yenye kipato kizuri.
Kimsingi,  cheti kazi yake ni kumpatia mtu kazi. Cheti ndio ‘pasipoti’ ya kwenda katika nchi ya kipato.
Watanzania wengi kama sio wote,  tumeangukia katika kundi hili. Wengi wetu tunataka pasipoti ya kwenda katika ‘nchi’ ya kipato cha kuajiriwa, tunataka vyeti!
Katika mfumo wetu wa elimu mpaka sasa ufaulu wa mtihani ndio unaosema fulani apangiwe shule gani, apangiwe kozi gani  chuoni, apate kiasi gani kwenye mikopo ya elimu ya juu na apangiwe kazi gani na alipwe kiasi gani.
Sasa kuna vita kati yetu, kila mmoja anataka mwanawe, yeye mwenyewe au ndugu yake  afaulu ili afike katika nchi ya ahadi.
Mbinu mbalimbali zinatumika  kufanikisha lengo hili, vita haina macho! Mbinu kuu ikiwa matumizi ya pesa. Kusoma shule nzuri na ghali, kulipia twisheni, walimu bora, kununua vitabu na mwishowe hata kununua mitihani.
Mchakamchaka  huu wa kutaka kufaulu kisha kupata vyeti,  unawaacha nyuma watu wa kipato cha chini kwani hawawezi kumudu kununua mitihani, au kusoma twisheni  za gharama.
Wenye nacho wananeemeka na mtindo huu. Mwelekeo unaonyesha masikini  wataachwa kwa kiasi kikubwa na wenye uwezo.
Mwanzo wa kujenga matabaka mawili kupitia elimu bila kificho  unaonekana.

Alhamisi hii feb 7,2013 kwenye AMPLIFAYA Clouds Fm.

Alhamisi hii feb7 2013 kuanzia saa moja usiku kwenye AMPLIFAYA ya CLOUDS FM dakika 120 zitatumika kuirusha Exclusive interview ya BABU WA LOLIONDO, ni safari iliyochukua dakika 570 kutoka Arusha mjini, ni zaidi ya saa masaa tisa(9).
Safari ya kwenda kwa Babu wa Loliondo Samunge ilianza kwenye defender ya polisi kwa sababu magari ya watu binafsi yalikua yanagoma kwenda kutokana na vita kali ya Wasonjo na Wamasai, hivyo njia pekee ya kufika kwa Babu ni kusindikizwa na Polisi, stori kamili ni Alhamisi hii feb 7 2013 kwenye AMPLIFAYA Clouds Fm.
Kwenye interview ya zaidi ya dakika 60 na Babu wa Loliondo Ambilikile, picha na stori nyingine zitapatikana kwenye millardayo.com kuanzia jumatano usiku na alhamisi.

kikao kazi cha maafisa habari wa serikali Dodoma

Picha na 1 f90c5Waziri wa Habari, Vijana ,Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara akifungua mkutano wa maafisa Habari, Elimu na Mawasiliano wa serikali mjini Dodoma. Pamoja na mambo mengine amewataka kufanya kazi  kwa kuzingatia weledi na kutoa taarifa sahihi kwa umma mara kwa mara kuhusu shughuli mbalimbali zinazofanywa na serikali.


Picha no 8 03ec7
 Mmiliki na muendeshaji wa mtandao wahabari na matukio wa Mjengwa Blog kutoka Iringa Bw. Maggid Mjengwa akitoa mada kwa maafisa Habari, Elimu na Mawasiliano wa serikali kuhusu Faida na Changamoto za matumizi ya mitandao ya kijamii kwa Mawasiliano Serikalini mjini Dodoma.


Picha na 7 f660a
Maafisa Mawasiliano wa Serikali wakiendelea na kikao kazi chao kujadili masuala mbalimbali ya utendaji kazi Mjini Dodoma.


Picha na 2 5c000
Maafisa Habari, Elimu na Mawasiliano wa Serikali wakiwa katika picha ya pamoja naWaziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo mara baada ya ufunguzi wa kikao kazi hicho  mjini Dodoma.


Picha na 3 958db
Afisa Habari wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi wa Hesabuza Serikali  Sarah Reuben akichangia moja ya mada katika kikao kazi cha Maafisa Habari, Elimu na Mawasiliano wa Serikali mjini Dodoma.


hab1 55f16
Baadhi ya maafisa habari wa serikali wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiAwasilishwa katika mkutano huo. Kutoka kulia ni Bw. Peter Millanzi mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Bw. Midradji Maez, Mkuu wa kitengo cha mawasiliano Shirika la Reli Tanzania (TRL) na Bw. Abel Ngapemba, Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano Shiririka la Maendeleo la Taifa NDC


hab2 6bb7f
. Maafisa Habari kutoka wilaya na Mikoa mbalimbali waliohudhuria kikao kazi cha maafisa habari mjini Dodoma wakiwa katika majadiliano ya pamoja kuhusu mafanikio na changamoto zinzoyakabili maeneo yao ya kazi.


hab3 bf999
Maafisa Habari kutoka wizara mbalimbali waliohudhuria kikao kazi cha maafisa habari mjini Dodoma wakiwa katika majadiliano ya vikundi kuhusu mafanikio na changamoto zinazoyakabili maeneo yao ya kazi wakiongozwa na mwenyekiti wa kikundi hicho Luteni Kanali Juma Sipe, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano.


hab 50c83
Meneja Mawasiliano wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Bw. Innocent Mungy akiwasilisha mada kuhusu mkakati wa Mawasiliano wakati wa Kikao kazi cha maafisa habari wa serikali kinachoendelea mjini Dodoma.

5/2/2013, Dodoma
Kikao kazi cha Maafisa habari wa Serikali kutoka Wizara, taasisi, wakala wa serikali, mashirika ya umma, mikoa na wilaya mbalimbali nchini leo kimeingia siku ya pili mjini Dodoma kwa  maafisa hao kupata fursa ya kujadili changamoto zinazokabili vitengo vya  habari na mawasiliano serikalini na namna ya kuzitatua.
Katika kikao hicho mada mbalimbali zimewasilishwa ikiwemo ile ya Mwongozo wa Ofisi za Mawasiliano serikalini iliyowasilishwa na Mkurugenzi wa Msaidizi kutoka Idara ya Habari (MAELEZO) anayeshughulikia uratibu wa vitengo vya mawasiliano serikalini akitoa msisitizo mkubwa  kwa maafisa habari kuyafahamu vizuri majukumu yao ya kazi kwa mujibu wa taratibu za utumishi wa umma ili kuboresha utendaji wa kazi.
 Pia maafisa hao wamepata fursa ya kujifunza namna ya kuboresha  mawasiliano serikalini kupitia mada ya mkakati wa mawasiliano (Communication Strategy) wa kuiwezesha jamii kupata taarifa sahihi kwa muda muafaka ,mada iliyowasilishwa na Meneja mawasiliano kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Bw. Innocent Mungy.
Katika mada hiyo Bw. Mungy ametoa wito kwa maafisa hao kuzitumia nafasi zao kutoa taarifa kwa umma mara kwa mara ili kuwapa fursa wananchi kufahamu yale yanayofanywa na serikali.
Ametoa wito maafisa hao kushirikiana na vyombo mbalimbali vya habari katika kutekeleza mkakati huo kwa kuhakikisha kuwa wanatoa habari kwa umma kupitia radio, magazeti, televisheni na mitandao ya kijamii ili kuepusha madhara yanayoweza ku.sababishwa na jamii kukosa taarifa sahihi za serikali za utekelezaji wa mipango mbalimbali ya maendeleo

Friday, February 1, 2013

polisi Mtwara wakimbia makazi

Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU)  katika ubishi Mtwara hivi karibuni

SHINIKIZO la wananchi mkoani Mtwara kutaka gesi isitoke mkoani humo, limesababisha polisi takriban 50 kuzikimbia familia zao baada ya kutishiwa maisha na wananchi.

Habari za kuthibitishwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Maria Nzuki zimeeleza kuwa polisi hao ambao wengi wao ni wale wanaoishi mitaa mbalimbali mjini humo, wamehamia kambini kutokana na kutishiwa maisha na wananchi kwamba watawadhuru wao na familia zao.

Habari hizo zilieleza kuwa, vurugu zilizotokea Januari 25 na 26, mwaka huu na kusababisha vifo vya watu wanne huku jengo la Mahakama ya Mwanzo na nyumba zikiwamo za wabunge kuchomwa moto na nyingine kuharibiwa vibaya, ni moja ya sababu zilizowatisha polisi hao.
“Wamerudi kambini kwa sababu ya kutishiwa ila ni baadhi ya askari, siyo wote,” alisema kamanda huyo.

Juzi, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alisema hasira za wananchi hao ni kudhani kuwa gesi hiyo itapelekwa wilayani Bagamoyo nyumbani kwa Rais Jakaya Kikwete.
Alisema pia mpasuko ndani ya CCM mkoani humo na harakati za kisiasa ni sababu nyingine zilizochochea mgogoro huo.

Hata hivyo, Kamanda Njuki alisema hana idadi kamili ya askari waliokimbia makazi yao huku akifafanua kuwa mambo yatatulia mkoani humo ikiwa Serikali itatekeleza ahadi zake.
“Serikali inatakiwa kutekeleza ahadi zake ilizozitoa kwa wananchi ili kuweka hali shwari, lakini pamoja na hayo sisi tutaendelea na ulinzi kuhakikisha kuwa kila kitu kinakwenda sawa na hali inakuwa shwari,” alisema Njuki.

Alisema baadhi ya wananchi wamekuwa wakiwatisha polisi hao na kutokana na hali hiyo imeonekana ni vyema waende kambini.

Askari wengi waliokimbia nyumba zao ni wale ambao makazi yao yanafahamika na wananchi ambao wakati wa vurugu hizo, walikuwa miongoni mwa askari waliokuwa waki zituliza. Inaelezwa kwamba wapo polisi zaidi ya 40 ambao hawaonekani mtaani na hata katika nyumba wanazoishi.

“Hivi sasa hawapo, si unaona mji ulivyokuwa mweupe, watu wana hasira na wanataka gesi isitoke, kwa hiyo hata wakimwona polisi wanaweza kumfanya lolote,” alisema mtoa habari ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini na kuongeza:

“Wananchi sasa wamekuwa kitu kimoja, wameweka siasa na tofauti zao nyingine kando kutaka gesi iwanufaishe, ila binafsi naomba jambo hili limalizike kwa amani.”

SIRI YA MGOGORO WA GESI MTWARA YAFICHUKA

MTWARA KUMEKUCHA: SIRI YA MGOGORO WA GESI MTWARA YAFICHUKA: MOJA ya mambo yaliyoamsha hisia za wakazi wa Mkoa wa Mtwara hadi kushinikiza kwa vurugu wakitaka gesi isitoke mkoani humo, ni taarifa kuwa...

TASWIRA YA MTWARA
 uwanja wa ndege


 mtwara posta


hekaheka za kushinikiza kwa vurugu wakitaka gesi isitoke mkoani humo


fanya fujo uone



kumekucha
 

 juhudi