Thursday, December 6, 2012

darasa la kwanza na la pili waendelea kusomea kwenye darasa moja kutokana na uhaba wa vyumba vya madarasa unaoikabili Shule ya Msingi, yenye darasa la kwanza hadi la saba.

Hili ni darasa jipya lililojengwa sasa katika Shule ya Msingi Silabu iliyopo Wilaya ya Korogwe darasa hili linatumiwa na wanafunzi wa darasa la tatu



Mti huu kivuli chake ni ofisi ya walimu wa Shule ya Msingi Silabu iliyopo Wilaya ya Korogwe
 

Uchochoro huu ndio lililuwa darasa la tatu kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Silabu iliyopo Wilaya ya Korogwe


Na Mwandishi wa Thehabari.com Korogwe WALIMU wa Shule ya Msingi Silabu Wilayani Korogwe Mkoa wa Tanga bado wanatumia kivuli cha mti uliopo mbele ya shule hiyo kama ofisi ya walimu (staff room) kwa kukosa jengo la ofisi. 
Hiki ni kipindi cha miezi sita imepita sasa tangu mtandao wa Thehabari.com uripoti habari hii mapema mwezi Agosti 2012. Juzi mwandishi wa habari hizi alipita tena katika shule hiyo kuangalia juhudi za Serikali na wananchi kufanikisha ujenzi wa ofisi hiyo, lakini alishuhudia walimu wa shule hiyo wakiendelea kufanya shughuli zao chini ya mtimu.
 “…Hii ndiyo ofisi yetu bado,jengo ambalo tutalitumia kama ofisi halijajegwa shuleni hapa, hivyo tunatumia kivuli cha mti huu kama ofisi na wakati mwingine jua likizidi huamia pembezoni mwa kingo za darasa lenye kivuli,” alisema mmoja wa walimu ambaye alikutwa amekaa chini ya mti huku akiendelea na kazi. 
Hata hivyo mwalimu huyo hakuwa tayari kutaja jina lake kwa madai si msemaji wa shule hiyo, juhudi za kumpata Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Silabu, Mizeki Charahani ziligonga ukuta baada ya kuambiwa alikuwa nje ya shule kikazi. 
Awali mwezi Agosti mwandishi wa habari hizi aliripoti wanafunzi wa darasa la tatu katika Shule hiyo kusomea kwenye uchochoro unaotenganisha kati ya darasa moja na lingine kutokana na uhaba wa vyumba vya madarasa. Wanafunzi hao ambao darasa lao lilikuwa likihama kila muda kutengemea hali ya hewa (jua na mvua) kufuata kivuli walilazimika kusomea nje kwenye uchochoro ambao haujaezekwa kutokana na uhaba wa vyumba vya madarasa shuleni hapo. 
 Hata hivyo tayari limejengwa darasa moja ambalo kwa sasa linatumiwa na wanafunzi wa darasa la tatu, huku darasa la kwanza na la pili wakiendelea kusomea kwenye darasa moja kutokana na uhaba wa vyumba vya madarasa unaoikabili shule hiyo, yenye darasa la kwanza hadi la saba. 
*Imeandaliwa na www.thehabari.com

No comments:

Post a Comment