Thursday, February 14, 2013

JK awapa polisi ‘meno’ kudhibiti maandamano

“Wajibu wenu umetajwa kisheria, mamlaka yenu mlikabidhiwa na Bunge na wanapopiga kelele kuwa mmetumia nguvu kubwa, waambie sheria mmezitunga ninyi kwa hiyo nendeni mkazibadilishe,”

Aliwaagiza polisi kutimiza wajibu wao kuhakikisha wanadhibiti vurugu zote bila ya kusikiliza maneno ya wanasiasa na watu wengine, ambao wanalaumu bila  kujua kazi nzuri inayofanywa na askari.
“Wajibu wenu umetajwa kisheria, mamlaka yenu mlikabidhiwa na Bunge na wanapopiga kelele kuwa mmetumia nguvu kubwa, waambie sheria mmezitunga ninyi kwa hiyo nendeni mkazibadilishe,” alisema Rais Kikwete.
Pia, Rais Kikwete alishangazwa na  kauli za watu kuwa, polisi wanatumia nguvu kubwa kupita kiasi, lakini hajajua tafsiri hiyo inacholenga.
Aliwaagiza polisi kufanya kazi kwa uweledi na kujituma zaidi kulingana na mafunzo waliyoyapata kutoka vyuoni, ikiwamo  kutafuta jinsi bora ya kuzuia machafuko hata kabla ya kutokea.
Akitaja baadhi ya vyanzo vya vurugu hizo, alisema ni kutokana na baadhi ya wanasiasa kushindwa kutii maagizo ya polisi hata pale wanapozuiwa kufanya mikutano.
Awali, Mkuu wa Polisi nchini, Said Mwema alisema wanaendelea  kuratibu na kusimamia mikakati  kuhakikisha wanakuwa wa kisasa zaidi.

No comments:

Post a Comment