Thursday, October 25, 2012

Bidhaa mbovu za mamilioni zimeteketezwa Tanga

 https://encrypted-tbn1.gstatic.com/images?q=tbn:ANd9GcSpn9qRNrd-Bi6ms828JKLA-I-rYsm4-JbEDmYFuCtSA6g2nNee
Raisa Said,Tanga.
HALMASHAURI ya  Jiji la   Tanga,  imeziteketeza  dawa, vipodozi  na bidhaa za vyakula ambavyo muda wa kutumiwa kwake, umekwisha.Kwa pamoja, bidhaa hizo zina thamani ya  Sh. 13.908,730.

 Akizungumza  na waandishi  wa habari mara  baada  ya  tukio hilo,  Kaimu  Mfamasia  wa Jiji  la  Tangam Abdillah Mnenge,  alisema dawa hizo zilikamatwa kutoka kwa wafanyabiashara mbalimbali wa jijini hapa .

Mnenge alisema  uteketezaji wa dawa hizo, ulifanyika juzi katika dampo kubwa lililoko Duga Maforoni na kwamba ulisimamiwa na wataalamu kutoka katika halmashauri ya Jiji na askari polisi.
Aliiomba Serikali kupitia Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) kuimarisha mipaka na ukaguzi ili kudhibiti uingizwaji wa vipodozi haramu hapa nchini.

Pia aliviomba vyombo vya habari hapa nchini, kutoa elimu juu ya madhara ya utumiaji wa bidhaa ambazo si rafiki wa binadamu na zilivyokwisha muda wake.

Kaimu Mfamasia huyo alisema wataendelea kuimarisha i ukaguzi kila baada ya miezi mitatu katika maeneo yote ya Halmashauri ya Jiji la Tanga, ili kudhibiti uingizwaji wa bidhaa zilizokwisha muda wake.

No comments:

Post a Comment