Saturday, December 29, 2012

Magufuli Amteua Prof Ninatubu Lema Kuwa Mwenyekiti Wa Bodi (ERB)

Prof Ninatubu Lema kutoka Chuo cha Uhandisi na Teknolojia (CoET), kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB)

 
WAZIRI wa Ujenzi, John Magufuli amemteua  Prof Ninatubu Lema kutoka Chuo cha Uhandisi na Teknolojia (CoET), kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB), uteuzi huo unaanzia Desemba 20 mwaka huu.
 
Kwa mujibu wa taarifa ya Magufuli iliyosambazwa kweye vyombo vya habari jijini Dar es Salaam jana, na kusainiwa na Kaimu Katibu Mkuu, Balozi Herbet Mrango, ilieleza kuwa uteuzi huo, utadumu kwa kipindi cha miaka mitatu hadi Desemba 20, 2015.
 
Kwa mujibu wa sheria Na. 15 ya mwaka 1997 ya mabadiliko madogo ya sehemu ya 3(3) ya kifungu 1(1) (a), na 1(2), kama ilivyorekebishwa na Sheria Na. 24 ya mwaka 2007, ndiyo iliyomfanya Waziri afanye uteuzi wa wajumbe wa Bodi hiyo akiwemo mwenyekiti huyo.
 
Katika uteuzi huo, Magufuli pia aliwataja wajumbe wanane wa bodi hiyo ya ERB, kuwa ni pamoja na Fintan Kilowoko kutoka wizara hiyo, ambapo kwa sasa ni mkurugenzi wa Barabara za Mikoa, Joseph Malongo, ambaye kwa sasa ni Msajili Msaidizi Huduma za Usajili na Gemma Modu kutoka Baraza la taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE), Nuberis Nyange kutoka Chama cha Wahandisi Washauri nchini (ACET).
 
Wengine ni Sarah Barahamoka, kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Edwin Ngonyani kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Prof Bakari Mwinyiwiwa; Mhandisi Mwandamizi, Chuo cha Uhandisi na Teknolojia (CoET), kutoka Chuo Kikuu cha Dar es salaam na Prof. John Kandoro; Mkuu wa Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT).
 
Waziri alisema kuwa jukumu la msingi la Bodi hiyo ya Usajili wa Wahandisi ni kusajili wahandisi pamoja na Kampuni zinazotoa ushauri wa kihandisi, kuendeleza wahandisi kitaaluma, kuwajengea uwezo wa Wahandisi wa kitanzania.

No comments:

Post a Comment