Friday, December 28, 2012

Umoja Wa Makanisa Nchini Kuliombea Taifa Disemba 31 Uwanja Wa Taifa

NA : MWANDISHI WA FULLSHANGWE-DAR ES SALAAM

MUUNGANO wa Makanisa nchini unatarajia kufanya Mkesha wa kuliombea Taifa ili amani na utulivu uliopo uweze kudumu, ambao unatarajiwa kufanyika Desemba 31 mwaka huu kwenye viwanja vya Taifa jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na wandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi, Godfrey Malassy , alisema mkesha huo umekuwa ukifanyika kila Desemba 31 ya kila mwaka, kuukaribisha mwaka mpya.
 
Alisema lengo la mkesha huo ni kuliombea Taifa hilo mungu, ili aweze kuliponya na kulinusuru na majanga mbalimbali, na kudumisha amani miongoni mwa jamii yote nchini.
 
Malassy aliongeza kuwa Taifa kwa sasa linapita katika kipindi kigumu hususani kuanzia uelewa, uchumi, na katika masuala ya usalama wa raia wa ndani na nje ya nchi ambapo kuna baadhi ya watu wameanza kuichezea amani kwa kusababisha vurugu kwa kvisingizio vya dini.
 
Pia alisema kuwa Watanzania wanapaswa kudumisha amani na utulivu kwani hiyo ni tunu ambaayo wamepatiwa na mungu hivyo haipaswi kuchezewa na watu wachache wasio na nia njema.
 
“Mkesha wa dua hilo, utafanyika Desemba 31 mwaka huu kuanzia saa 2:00 usiku hadi asubuhi katika viwanja vya Taifa Dar es Salaam, na tunatarajia Rais Jakaya Kikwete atakuwa mmoja wa wageni wetu waalikwa” alisema Malassy.
 
Malassy alibainisha kuwa mkesha huo wa maombezi utashirikisha mikoa zaidi ya 16 ya Tanzania Bra na Visiwani, ambapo utakuwa na lengo la kuwaleta Watanzania kuliombea Taifa kwa ajili ya kudumisha amani, umoja na mshikamano visitetereke.

No comments:

Post a Comment